WAZIRI WA AFYA MH. JENISTA MHAGAMA LEO AMETEMBELE KATIKA TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD

      Comments Off on

WAZIRI WA AFYA MH. JENISTA MHAGAMA LEO AMETEMBELE KATIKA TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD

Waziri wa afya Mh. Jenista Mhagama leo ametembele katika Taasisi ya Saratani Ocean Road kuona huduma za Tiba mionzi zinavyoendelea katika Taasisi hiyo.

Mh. Mhagama amejionea mashine za Linac na Colbat ambazo zinatumika katika kutoa huduma ya Tiba mionzi kwa wagonjwa wa Saratani.

Ikiwa Taasisi ya saratani Ocean Road Ina mashine mbili za Linac na moja kati ya hizo bado inahitilafu.

Aidha Mhe. Mhagama amesema wakati akizungumza na wananchi waliokuwa wanasubili matibabu amesema serikali ipo mbioni kuongeza mashine nyingine ya Tiba mionzi ili kuondoa shida zinazotokana kwa kuharibika kwa mashine.

Aidha upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Julius Mwaiselage ameishukuru serikali kwa kufanya mchakato wa kuongeza mashine nyingine ya Tiba mionzi itakayokuja hivi karibuni.