Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa walimbatana na Balozi wa India nchini Tanzania

      Comments Off on

Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa walimbatana na Balozi wa India nchini Tanzania

Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa walimbatana na Balozi wa India nchini Tanzania pamoja na wawakilishi wa kutoka Hospitali mbalimbali nchini India mapema leo wametembelea katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road na kujionea namna shughuli zilivyofanyika katika kufikia malengo waliyojiwekea.

Akizungumza wakati anawasilisha andiko la namna ambavyo Taasisi hii imefanya katika utoaji huduma zake, mkurugenzi mtendaji wa Taasisi hiyo amesema kuwa serikali ya Tanzania inajotahidi vya kutosha kutoa vifaa mbalimbali ambapo hata uwiano wa upimaji kwa wananchi kwa kiasi umeongezeka kutokana na kuimarishwa kwa shughuli za kimaabara ingawa pamoja na yote hayo bado

Taasisi inahitaji kuwekeza zaidi ili kiweza kufikia malengo ya kufikia watu wengi zaidi Tanzania na Nchi za njeUmoja wa nchi za kiarabu pamoja na nchi ya India kwa pamoja wanatembelea hospitali na taasisi kadhaa kuweza kupata changamoto na kuona namna gani wanaweza kuzitatua changamoto hizo ili kuweza kutoa matibabu yenye hadhi ya kimataifa.Aidha muungano huo umekubaliana kuwekeza kwa pamoja kwenye sekta ya Afya ili kuweza kuisaidia serikali ya Tanzania kwa kuokoa pesa nyingi ambazo hutumika katika kusaidia wananchi wake kwenda kutafuta matibabu zaidi nje ya nchi.