Ocean Road yaweka kambi siku sita, mafunzo na uchunguzi saratani ya kizazi – Tabora

      Comments Off on

Ocean Road yaweka kambi siku sita, mafunzo na uchunguzi saratani ya kizazi – Tabora

Baadhi ya wataalamu wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), iliyopo Jijini Dar es Salaam, wapo mkoani Tabora kwa kambi ya siku sita inayojumuisha mafunzo sambamba na uchunguzi wa awali wa saratani ya shingo ya kizazi.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa, Mkurugenzi wa Huduma za Kinga za Saratani ORCI, Crispin Kahesa amesema kambi hiyo imedhaminiwa na Bank ya NBC.

“Timu ya Wataalamu kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road tumeweka kambi mkoani Tabora kuanzia Juni 24 hadi 29, 2021. Tunatoa mafunzo ya uchunguzi wa awali wa saratani ya mlango wa kizazi,” amebainisha Kahesa ambaye ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani ORCI.

Amesema jumla ya watoa huduma wa afya 21 kutoka hospital, ‘dispensary’ na vituo vya afya vya Mkoa wa Tabora watanufaika na mafunzo kupitia kambi hiyo.

Ameongeza “Huduma ya uchunguzi wa awali wa saratani ya kizazi inafanyika bila malipo kwa wananchi wote