Kikao cha pili cha Baraza la Tano la Wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road. Ukumbi wa Edema, Morogoro 04/06/2021

      Comments Off on

Kikao cha pili cha Baraza la Tano la Wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road. Ukumbi wa Edema, Morogoro 04/06/2021

Wajumbe wa Baraza la tano la wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road walikutana na kufanya mkutano wa pili wa mwaka 2020/2021 katika ukumbi wa mkutano wa Edema mkoani Morogoro kwa ajili ya kupokea ripoti ya utekelezaji, muhtasari wa bajeti iliyopitishwa na kusomwa bungeni na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Dorothy Gwajima (mb) na mwenendo wa utoaji wa huduma za uchunguzi, tiba, kinga na tafiti.

Mapendekezo kutoka kwa wajumbe wa baraza la wafanyakazi yakiwemo uboreshaji wa utoaji wa elimu zaidi kwa umma kupitia redio, luninga, mitandao ya kijamii pamoja na kuwatembelea wahudumu wa afya mikoani na wilayani. Mafunzo haya yajumuishe pia wataalamu wa huduma anuai katika Taasisi wanaohudumia wagonjwa kama wakufunzi kutokana na ujuzi walioupata katika utoaji huduma. Mafunzo haya yatawezesha rufaa ambazo si muhimu kuratibiwa na kufanyiwa kazi kuanzia katika ngazi za wilaya. Pia iwezeshe hata wale wagonjwa wanaoruhusiwa kutoka Ocean Road kuweza kupatiwa huduma bora wawapo wilayani kwao na si kunyanyapaliwa.

Maboresho mengine yaliyopendekezwa kwa upande wa kitengo cha ufundi (estate) katika kuharakisha utekelezaji wa majukumu yao ya utoaji wa huduma za kiufundi kwa ubobezi na kiufanisi.