TUTASHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZOTE ZA SARATANI – MH. UMMY MWALIMU

      Comments Off on

TUTASHUGHULIKIA CHANGAMOTO ZOTE ZA SARATANI – MH. UMMY MWALIMU

Mh. Ummy Mwalimu ameahidi kushighulikia changamoto zozote zitakazojitokeza za Saratani katika nchi ya Tanzania ikiwamo na uwekaji wa mikaka madhubuti ili kuweza kuudhi its ugonjwa huo.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi taarifa ya kiuchunguzi iliyofanywa na Lancet Oncology katika ukumbi wa mikutano kwenye hoteli ya Hyatt Regency, mapema mwanzoni mwa wiki hii, waziri mwalimu amesema kuwa kiwango cha watu wanaopoteza maisha kutokana na Saratani ni kikubwa mno ukilinganisha na kile cha UVICO-19, kwani kwa mwaka 2020 pekee watu zaidi ya 25,000 wamepoteza maisha, huku ikikadiriwa kuwa idadi hiyo kuongezeka hadi kufikia watu 1,000,000 kw mwaka ifikapo 2030.

Waziri Mwalimu a.esema kuwa kutokan na takwimu hizo, serikali itaweka mikakati mahususi kuhakikisha tatizo hilo linatowekaKatika hatua nyingine, waziri mwalimu amesema kuwa serikali ipo katika mpango wa kutudisha tena chanjo kwaajili ya wasichana wa kua zia umri wa miaka 9-14 kujikinga na Saratani ya Mlango wa Kizazi.Akizungumzia zaidi jambo hilo, waziri mwalimu ametanabaisha kuwa chanjo hiyo ni kweli imeonekana kusua sua kutokana na baadhi ya watu kusema kuwa chanjo hiyo ina madhara makubwa ikiwamo kutopata ujauzito na matatizo mengine ya Afya ya uzazi hali ambayo sio kweli, kwani serikali imefanya uchunguzi na kujiridhisha kuwa chanjo hizo ni salama kabisa hivyo wataendelea kutoa chanjo hizo ili kunusuru maisha ya watoto hao kutokana na Saratani