54 WAKUTWA NA VIASHIRIA VYA SARATANI ARUSHA.

      Comments Off on

54 WAKUTWA NA VIASHIRIA VYA SARATANI ARUSHA.

Idadi ya watu 54 wamekutwa na viashiria vya Saratani mbalimbali katika kampeni ya uchunguzi wa awali wa Saratani jijini Arusha.

Akizungumza katika kampeni hiyo, Meneja kitengo cha uchunguzi wa Saratani, Dkt Maguha Stephano amesema kuwa idadi hiyo imetokana na uchunguzi wa Saratani ya Mlango wa kizazi kwa wateja 221 huku wale waliojitokeza kwaajili ya Saratani ya matiti wakiwa ni 257 na wale wa Tezi dume ni 362.Katika hatua nyingine Dr. Maguha amewahimiza wananchi wa eneo Hilo na maeneo mengine kwa ujumla kuhakikisha kuwa wànakuw na mtindo bora wa maisha ikiwa ni pamoja na kula matunda kwa wingi katika milo Yao yote.

Vile vile amewaasa kupunguza vyakula vyenye mafuta huku akiwasisitizia kufanya mazoezi mara kwa mara huku wakitakiwa kutumia vilevi kwa kiasi kidogo kama sio kuacha ili kuepukanaa na athari za magonjwa ya saratani.Kampeni hii imedumu kwa muda wa siku nne kuanzia tarehe 24 – 27 ya mwezi huu wa tisa