UCHUNGUZI WA MAPEMA WA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI PAMOJA NA CHANJO YA PAPILLOMA VIRUS ITASAIDIA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI

      Comments Off on

UCHUNGUZI WA MAPEMA WA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI PAMOJA NA CHANJO YA PAPILLOMA VIRUS ITASAIDIA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI

“Uchunguzi wa mapema wa Saratani ya mlango wa kizazi pamoja na chanjo ya papilloma virus itasaidia katika mapambano dhidi ya Saratani ya mlango wa kizazi”.

Hayo yamesemwa na mtaalamu kutoka University of Calfornia, San Diego Dkt. Chiku Nwachukwu leo wakati anawasilisha mada inayozungumzia mionzi Tiba ya ndani kwa njia ya kisasa kwa Saratani ya mlango wa kizazi ( 3D Brachytherapy In Cervical Cancer).

Dkt. Nwachukwu amefafanua namna njia hiyo ya kisasa inavyoweza kuleta matokeo Bora zaidi katika matibabu hayo ya Saratani ya mlango wa kizazi.

Kwa upande wa waliohudhuria katika mafunzo hayo, wamepata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali kuhusiana na tiba hiyo ya kitaalam ambapo kila mmoja slipata majibu kutoka kwa wataalam mbalimbali wa tiba hiyo waliojitokeza.

Ikumbukwe kuwa Taasisi ya Saratani Ocean Road imekwisha anza kutoa huduma ya mionzi tiba ya ndani kwa njia ya kisasa kuanzia mnamo mwezi wa Tano mwaka 2023.