TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD MAPEMA LEO IMEPOKEA TUZO YA HESHIMA YA KUTAMBUA MCHANGO WAKE KATIKA KUONA NAMNA GANI IMESHIRIKI KWENYE KUTOA ELIMU…

      Comments Off on

TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD MAPEMA LEO IMEPOKEA TUZO YA HESHIMA YA KUTAMBUA MCHANGO WAKE KATIKA KUONA NAMNA GANI IMESHIRIKI KWENYE KUTOA ELIMU…

Taasisi ya Saratani Ocean Road mapema leo imepokea tuzo ya heshima ya kutambua mchango wake katika kuona namna gani imeshiriki kwenye kutoa elimu, kufanya uchunguzi pamoja na matibabu ya magonjwa hayo.

Tuzo hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba wa Wizara ya Afya Prof. Paschal Rugajo wakati wa mkutano wa kimataifa wa kisayansi wa magonjwa yasiyoambukiza unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere.

Akizungumza wakati wa maonesho hayo leo mchana, Prof. Rugajo amesema kuwa katika kipindi hiki Taasisi ya Saratani Ocean Road imekuwa ikifanya vizuri sana kwenye utoaji wa tiba na hii imepelekea kuaminika na mataifa ya jirani na kupelekea kupata wateja wengi kutoka nje wakihitaji kuja kutibiwa hapa katika Taasisi hiyo.

Akisisitiza Prof. Rugajo
Amesema utoaji wa huduma bora ni chachu kubwa ya tiba utalii, na ndio kitu pekee ambacho kwa sasa Tanzania inaendelea kukitilia mkazo ili kuweza kupata matokeo chanya hususan kwenye sekta hii ya Afya.

Maonesho haya yatafanyika kuanzia leo tarehe 01/11/2023 mpaka siku ya Ijumaa tarehe 03/11/2023 katika kukuza ufahamu juu ya magonjwa haya yasiyoambukizwa kwa wananchi.