AFISA MIRADI WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA NGUVU ZA ATOMIC BI.AZA KASHLAN AMESEMA

      Comments Off on AFISA MIRADI WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA NGUVU ZA ATOMIC BI.AZA KASHLAN AMESEMA

Afisa miradi wa shirika la kimataifa la nguvu za Atomic Bi.Aza Kashlan amesema kuwa pamoja na msaada wa mashine walizozitoa kipindi cha nyuma, ila bado wataendelea na kutoa misaada mbalimbali ikiwemo mashine kwa namna itakavyowezekana ili kurahisisha matibabu katika Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Bi. Kashlan amesema mapema mwakani kutakuwa na mradi mwingine mkubwa ambao wanategemea pindi ukikamilika watauleta hapa katika Taasisi hii.

Akizungumza katika majadiliano maalum yaliyofanyika katika ukumbi uliopo ofisini kwake, mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt Julius Mwaiselage amesema kuwa ujio wa kiongozi huyu umempa nafasi ya kuzungumza nae mambo mbalimbali ikiwamo, kuanzisha shahada ya uzamili kwenye fizikia tiba, ununuzi wa vifaa mbalimbali vya kitabibu mfano, mashine za tiba n.k pqmoja na mafunzo upande wa uchunguzi kwenye mambo ya CT Scan.

Bi. Kashlan ameahidi kuitekeleza miradi yote ambayo Dkt. Mwaiselage amemuomba pindi tu muda utakapofikia kwa kuanzia na mambo kadhaa mapema mwakani.