Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt.Julius Mwaiselage leo amepokea msaada wa millioni arobaini kutoka Bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT).

      Comments Off on

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt.Julius Mwaiselage leo amepokea msaada wa millioni arobaini kutoka Bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT).

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt.Julius Mwaiselage leo amepokea msaada wa millioni arobaini kutoka Bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT).

Bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT) imetoa msaada huo katika kuadhimisha miaka ishirini ya Bodi hiyo ya michezo ya kubahatisha Tanzania.

Bodi hiyo imetoa bedside Mia moja zenye thamani ya Shilingi milioni ishirini na nne, Hundi yenye thamani ya Shilingi milioni kumi na tano pamoja na vifaa mbalimbali ikiwemo sabuni na maji.

Akitoa shukrani zake Dkt. Mwaiselage amesema msaada huo utakwenda kuimarisha maeneo ya ugonjwa, pamoja na kwa wagonjwa moja kwa moja.

Pia Dkt. Mwaiselage ameahidi msaada huo utakwenda pale ulipokusudiwa kwa Usimamizi madhubuti huku akitoa wito kwa wadau wengine kuleta misaada zaidi na milango ya Taasisi ipo wazi kupokea misaada mbalimbali.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bodi ya Michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT) Bw. James Mbalwe amesema katika kusaidia Jamii ni Jambo la lazima sio hiari, ndio mana wao wameamua kurudisha kile kidogo walichopata kwa jamii.

Bw. Mbalwe ameongeza kuwa kujitolea kwa kutoa misaada kwa pamoja italeta tija kubwa kwa Jamii inayotuzunguka.

Aidha Bodi hiyo ya Michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT) imeambatana na wadau wa michezo hiyo ya kubahatisha nchini katika kutoa misaada hiyo.