MAADHIMISHO YA WIKI YA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZWA

      Comments Off on

MAADHIMISHO YA WIKI YA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZWA

Naibu waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel akimsikiliza mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Julius Mwaiselage akizungumza kuhusu huduma zinazotolewa hapa Mnazi mmoja katika banda la Taasisi hiyo.

Leo ndio maadhimisho ya wiki ya magonjwa yasiyoambukizwa ambapo Taasisi ya Saratani Ocean Road ipo hapa Mnazi Mmoja ikitoa huduma za uchunguzi wa Saratani za Matiti, Mlango wa kizazi pamoja na Tezi dume bila malipo yoyote, hivyo watu wote wanakaribishwa kufanya uchunguzi huu.

Dkt. Mollel ndie mgeni rasmi wa maadhimisho hayo yanayofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja ambapo amekuja kumuwakilisha waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa kassim Majaliwa.