WAZIRI WA AFYA MH. UMMY MWALIMU AMEZINDUA RASMI BODI MPYA YA UDHAMINI KATIKA TAASISI YA SARATANI OCEAN ROADi

      Comments Off on

WAZIRI WA AFYA MH. UMMY MWALIMU AMEZINDUA RASMI BODI MPYA YA UDHAMINI KATIKA TAASISI YA SARATANI OCEAN ROADi

Mapema leo Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu amezindua Rasmi Bodi mpya ya udhamini katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo katika Taasisi ya Saratani Ocean Road.


Akizungumza katika uzinduzi huo Mheshimiwa Mwalimu amesema kuwa kati ya Taasisi zaidi ya 40 zilizo chini ya wizara ya Afya, Taasisi ya Saratani Ocean Road ipo katika Tatu bora kwa kutokuwa na makandokando ya lawama kutoka kwa Wananchi.
Aidha Waziri mwalimu ameushukuru uongozi wa bodi iliyoisha muda wake na kusema kuwa waliingia katika kipindi kigumu sana lakini waliweza kupambana kwa kuweka mipango sawa mpaka Taasisi kufikia hapa ilipo sasa.
Nae mkurugenzi wa Taasisi hiyo Dr. Julius Mwaiselage amepongeza jitihada zilizofanywa na uongozi uliopita ambao ulikuwa chini ya profesa Hamisi Dihenga kwa kuifikisha Taasisi hapa ilipo.


Profesa Dihenga amemaliza muda wake na kuteuliwa kuwa Mwenekiti wa bodi ya bodi ya mikopo nchini Tanzania na kumpisha Profesa Kaaya na timu yake ya watu nane kuiongoza bodi hiyo ili kusukuma gurudumu la utoaji huduma mbele