Mwezi wa Uelimishaji wa Saratani ya Matiti Duniani

      Comments Off on

Mwezi wa Uelimishaji wa Saratani ya Matiti Duniani

Mwezi wa Uhamasishaji wa Saratani ya Matiti, unaadhimishwa kote ulimwenguni ifikapo kila Oktoba, maadhimisho hayo hulenga kusaidia kuongeza umakini na msaada wa elimu kwa wanawake, ugunduzi wa mapema na pia huimarisha upatikanaji wa matibabu wa mapema wa ugonjwa huu baada ya kugundulika mapema.

Idara ya kinga na uchunguzi wa Saratani ya Taasisi ya Saratani Ocean Road pia, imeadhimisha mwezi wa uelimishaji wa Saratani ya matiti duniani. Oktoba inafahamika duniani kote kuwa ni mwezi maalumu wa kuadhimisha mapambano dhidi ya Saratani ya matiti.

Idara ya Kinga na Uchunguzi wa Saratani iliaandaa semina maalumu kwa wanawake mashujaa

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Dr. Mwaiselage akizungumza na washiriki wa semina

mnamo tarehe 01/10/2020 lenye dhumuni kuu la kuwapa elimu ya Kinga na ufahamu wa njia stahiki za kujichunguza au kufanyiwa uchunguzi wa awali wa saratani ya Matiti. Ujumbe mkuu wa maadhimisho ya mwezi huu ni ‘Ushirikiano wa pamoja katika kinga na tiba’.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Dr. Mwaiselage akizungumza na washiriki wa semina

Akizungumza na washiriki wa semina, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road alieleza kuwa, Kuna visa vipya milioni 1.38 na vifo 458,000 kutokana na saratani ya matiti kila mwaka (IARC Globocan, 2008) duniani kote. Saratani ya matiti ni saratani ya kawaida kwa wanawake ulimwenguni kote, katika nchi zilizoendelea na zinazoendelea. Katika nchi zenye kipato cha chini na cha kati matukio yamekuwa yakiongezeka kwa kasi katika miaka ya hivi karibuni kutokana na kuongezeka kwa umri wa kuishi, kuongeza ukuaji wa miji na ubadilikaji wa mitindo ya maisha kama ilivyo nchi za magharibi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Dr. Mwaiselage akizungumza na washiriki wa semina

Hivi sasa kuna ujuzi wa kutosha katika ugunduzi na tiba za saratani ya matiti, hata hivyo, kugundua mapema ugonjwa huo ni sababu kuu na ya msingi katika kudhibiti na kuitibu saratani ya matiti. Ikiwa saratani ya matiti inagunduliwa mapema, na ikiwa utambuzi na matibabu ya kutosha yanapatikana, kuna nafasi nzuri kwamba saratani ya matiti inaweza kuponywa na mgonjwa kuendeleza kuishi katika hali ya kawaida kabisa.

Dr Mwaiselage alitumia semina hilo, kutoa shukrani za dhati kwa Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa John Joseph Pombe Magufuli kwa kutekeleza kivitendo mipango kamili ya kudhibiti saratani kwa ununuzi wa vifaa tiba na sapoti inayoendelea katika miradi mipya na hali ya upatikanaji wa dawa za kutibu Saratani nchini na hasa hasa katika Hospitali ya Ocean Road

Wakizungumza na washiriki, watoa mada katika semina, Sister Mary Haule na Sister Genoveva Mlewa waliwaasa wanawake wote kujenga utaratibu wa kupima mapema. “Ikiwa itachelewa kugunduliwa, hasa inapokuwa katika hatua ya tatu na nne, hapo hulazimika kutibiwa kwa matibabu ya tiba shufaa, ambapo, utunzaji mzuri wa kupunguza mateso ya wagonjwa na familia zao hufanyika”. Kwa msingi huo, waliwaasa wanawake wote, kuweka utaratibu wa kujichunguza na kufika hospitalini mapema kuweza kuchunguzwa, na ili wanapobainika wapatiwe matibabu ya haraka na yenye manufaa

Akiongelea kuhusu madhara ya vifo, Mkurugenzi wa Idara ya Kinga na Uchunguzi, Dr Crispin Kahesa alisema, ”Vifo vingi (269,000) vinatokea katika nchi zenye kipato cha chini na cha kati, ambapo wanawake wengi walio na saratani ya matiti hugunduliwa katika hatua za mwisho kwa sababu ya ukosefu wa ufahamu juu ya kugundua mapema na vizuizi vya huduma za afya kwa mapema. Aliendelea kuwahimiza kina mama, kuratibu na kuhudhuria kliniki za uchunguzi wa Saratani mara kwa mara ili kujiepusha kuja kugundulika katika hatua za mwisho.

Mkurugenzi Idara ya Kinga, Dr. Kahesa akizungumza na washiriki wa semina

Katika maadhimisho ya mwezi huu, Taasisi ya Saratani Ocean Road, itaendelea na programu za uchunguzi na tiba za Saratani ya matiti kwa wanawake wote watakaofika katika kliniki ya uchunguzi na tiba iliyopo jengo la Block A. Tunawahimiza kwa wanawake wote kujumuika na kushirikiana na wahudumu wetu ili wapate kuchunguzwa na kujua mustakbali wa afya zao.

Upasuaji kuondoa uvimbe wa saratani bila kuondoa titi lote waleta ahueni kwa wagonjwa

Upasuaji wa kisasa wa kuondoa uvimbe wa saratani pasipo kuondoa titi lote lililoathirika umeleta ahueni kwa wagonjwa na kupunguza unyanyapaa nchini.

Yameelezwa hayo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), Dk. Julius Mwaiselage alipozungumza na waandishi wa habari katika mahojiano maalum, kuhusu mwezi Oktoba ambao ni maalum Kidunia kwa ajili ya uelimishaji, uhamasishaji, uchunguzi na matibabu ya saratani hiyo.

Mashujaa (wanawake waliotibiwa na kupona saratani ya matiti) na wale wanaoendelea na matibabu dhidi ya ugonjwa huo wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI Dk Julius Mwaiselage pamoja na  Mkurugenzi wa Huduma za kinga ya Saratani wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dk Crispin Kahesa wakiinua Mkono juu kuashiria kuishinda Saratani ya matiti

Amesema wastani wa wanawake 100 wanaogundulika na saratani hiyo ikiwa katika hatua za awali, huondolewa uvimbe kwa njia ya upasuaji pasipo kung’olewa titi lote lililoathiriwa, kila mwaka.

Amesema huduma hiyo ilianza kutolewa rasmi mwaka 2016 nchini na wataalamu wa ORCI wakishirikiana na wenzao wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH- Mloganzila).

Dk. Mwaiselage amebainisha kwamba ORCI kila mwaka huona wagonjwa wa saratani ya matiti kati ya 600 hadi 700 ambapo hao 100 ambao ni sawa na asilimia 30 hutibiwa kwa kuondoa uvimbe pasipo kung’oa titi lote.

“Zamani kwa kuwa hatukuwa na mashine za kisasa za tiba mionzi, matibabu yalikuwa ni lazima kuondoa titi lote, changamoto nyingine tuliyokuwa tunakabiliana nayo ni wagonjwa hawa kuchelewa kuja hospitalini, walikuja ugonjwa ukiwa umefikia hatua za juu mno, haikuwa rahisi kupata matokeo mazuri ya tiba.

Mashujaa (wanawake waliotibiwa na kupona saratani ya matiti) na wale wanaoendelea na matibabu dhidi ya ugonjwa huo wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI Dk Julius Mwaiselage (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao

“Lakini kutokana na maboresho yaliyofanywa na Serikali kwa kutumia mashine hii ya ‘Linear accelerator’, tunao uwezo wa kuchunguza na kutibu kwa kuondoa ule uvimbe tu na kuliacha titi, baada ya upasuaji huo mgonjwa anaendelea na matibabu ya mionzi kupitia mashine ya kisasa tuliyonayo hapa ORCI,” amesisitiza.

Amesema hata wale waliofanyiwa upasuaji na kuondolewa katika titi lote jitihada zinafanyika ambapo tayari wataalamu wapo nchini China wakijifunza jinsi ya kufanya upasuaji wa kupandikiza matiti.

“Corona imetuchelewesha, walikuwa wawe wameshamaliza masomo yao na kurejea nchini tayari kuanzisha huduma hii,” amebainisha.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratni Ocean Road, Dk Julius Mwaiselage akizungumza na mashujaa hao

Amesema Shirika la Afya Duniani (WHO) linakadiria kila mwaka Tanzania kuna wagonjwa wapya 42,000 wa saratani aina zote, saratani ya matiti inaongoza duniani kote kwa kuathiri wanawake kwa asilimia 99, wanaume asilimia moja.

“Tanzania saratani ya matiti inashika nafasi ya pili kwa idadi kubwa ya wagonjwa, miaka 10 iliyopita ilikuwa inashika nafasi ya nne, tunaona inaongezeka kwa kasi,” amebainisha.

Amesema changamoto ambayo wanaiona hivi sasa kwenye jamii ni wimbi la taarifa potofu zilizopo kwenye mitandao ya kijamii, baadhi ya wagonjwa hushawishiwa kwenda kupata dawa za kienyeji ambazo hata hazijafanyiwa utafiti na hivyo huacha tiba za hospitalini.

Mkurugenzi wa Huduma za kinga ya Saratani wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dk Crispin Kahesa akizungumza jambo katika semina ya siku moja kwa mashujaa wa saratani ya matiti.

Chanzo: https://matukionamaisha.blogspot.com/2020/10/

Parokia ya Kibamba waishukuru ORCI kuwapelekea huduma uchunguzi wa Saratani

      Comments Off on

Parokia ya Kibamba waishukuru ORCI kuwapelekea huduma uchunguzi wa Saratani

Waamini wa Kanisa Katoliki Mtakatifu Vincent wa Paulo, Parokia ya Kibamba, wamewashukuru wataalamu wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), kwa kuwapeleka huduma ya uchunguzi wa afya bila malipo.

Kanisa hilo jana liliadhimisha kumbukumbu ya Mtakatifu Vincent wa Paulo ambaye ni somo wa parokia. Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya waumini wa kanisa hilo, wamesema kufikishiwa huduma hizo za uchunguzi imekuwa jambo jema kwani wamepima na kujitambua afya zao.

“Tunasherehekea kumbukumbu ya Mtakatifu Vincent wa Paulo, Baba Paroko wetu, aliona vema wataalamu waje kanisani nasi tupate huduma za uchunguzi, nimefarijika mno, nimechunguzwa saratani ya kizazi na matiti bila malipo, nimeambiwa nipo vizuri, nina amani moyoni mwangu,” alisema mmoja wa waumini hao.

Muuguzi wa Kitengo cha Uchunguzi wa Saratani ORCI, Beatrice Mushi alisema waliwachunguza jumla ya waamini 168.

“Katika idadi hiyo 81 tuliwachunguza saratani ya matiti ambapo wawili tuliwakuta na uvimbe ni kiashiria cha awali cha saratani, 59 tuliwachunguza saratani ya kizazi watatu kati yao tuliwakuta na viashiria vidogo vya saratani na mmoja kiashiria kikubwa,” alisema.

Aliongeza “Kwa upande wa saratani ya tezidume waliochunguzwa ni wanaume 28 ambapo wawili kati yao tuliwakuta na viashiria vya saratani, tuliowakuta na viashiria tumewapa rufaa kuja kule kwenye taasisi yetu kwa uchunguzi zaidi na matibabu.

Awali wakati wa ufunguzi wa maadhimisho hayo, Paroko wa Kanisa hilo, Padre Prejo Joseph aliwashukuru wataalamu wote wa afya waliokubali kujumuika nao katika maadhimisho hayo pamoja na wataalamu wa masuala ya kisheria.

https://matukionamaisha.blogspot.com/

Dc. Jokate ahimiza jamii kutembelea, kuwafariji wagonjwa

      Comments Off on

Dc. Jokate ahimiza jamii kutembelea, kuwafariji wagonjwa

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegero amepokea msaada wa vifaa tiba vilivyotolewa na Jema Foundation kwa ajili ya wagonjwa wanaopatiwa matibabu ya saratani katika Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Taasisi hiyo inasimamiwa na Jema Baruani ambaye ni miongoni mwa wagonjwa waliowahi kutibiwa saratani Ocean Road na kupona sasa akijitolea kuendelea kuelimisha jamii kuhusu magonjwa hayo.

Akipokea msaada huo, amehimiza jamii kuendeleza utamaduni wa kuwatembelea, kuwajulia hali wagonjwa waliolazwa wodini, hospitalini walimolazwa ili kupatiwa matibabu dhidi ya maradhi mbalimbali yanayowakabili.

“Hakuna anayeijua kesho yake,” amesisitiza.

Dc jokate ametumia mfano hai wa shangazi yake ambaye alijiwekea utaratibu wa kuwatembelea na kuwasaidia wagonjwa pasipo kujua kwamba kitendo hicho siku moja kingekuwa msaada mkubwa kwake.

“Alikuwa anajitoa sana, kila alipotoka kazini aliwatembelea wagonjwa wa saratani, sasa hivi ni mstaafu, wakati alipokuwa anafanya vile hakuwahi kufikiri siku moja itakuwa sehemu muhimu ya kipenzi chake (mume wake), kwenda kutibiwa.

“Kwa hiyo, alipolazwa kwa matibabu, kwa kuwa yeye (shangazi) alikuwa tayari anafahamika, ilikuwa wepesi kusaidiwa pia. Tunayoyafanya sasa ni hazina ya maisha yetu ya baadae,” amesisitiza.

Amewapongeza Jema Foundation kwa kujitoa kwa jamii hususan wagonjwa wa saratani kwa kuwatembelea na kuwafariji kila mwaka.

“Nawapongeza madaktari na wataalamu wote wa Ocean Road kwa kazi kubwa wanayofanya ya kuwahudumia wagonjwa hawa,” amesema.

Ameongeza “Kipekee naipongeza Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imesimika vifaa vya kisasa hapa Ocean Road na sasa tunashuhudia inapokea wagonjwa wengine pia kutoka nje ya Tanzania.

“Daktari (Crispin Kahesa), amenieleza kwamba wanapokea wagonjwa kutoka nje ya nchi kwa sababu kuna uwezekaji mkubwa umefanywa na Serikali kwa kusimika mashine ambazo wenzetu kwenye nchi zao hawana.

“Amenieleza, huduma za tiba ya saratani zinayopatikana Tanzania ni bora za viwango vya kimataifa na gharama ni nafuu kulinganisha na mataifa mengine.

“Haya ni mambo ambayo lazima tuwaambie Watanzania, wajue kwamba tuna vitu ambavyo wengine wanatamani kuwa navyo, waje wapatiwe huduma bora,” ametoa rai Mkuu huyo wa Wilaya.

Mwakilishi wa Jema Foundation, Jema Baruani amesema wagonjwa wengi wa saratani huwa na hofu pale wanapogundulika, wapo wengine ambao huacha matibabu.

“Si wote huwa na moyo wa ujasiri kama mimi, wapo wanaokata tamaa,  si wote wana uwezo wa kulikabili gonjwa hili, inabidi sisi ambao Mungu ametujalia, tujitoe katika hali na mali, kuwaona… unaweza ukaja hapa japo kuwaambia neno pole, ikawa ahueni kwao,” amesema.

Jema ametoa rai pia kwa jamii hususan vijana kuwa na ujasiri na kujitokeza kufanyiwa uchunguzi wa saratani kwani ikiwa kugundulika, mtu hupona baada ya matibabu.

Mkurugenzi wa Kinga wa ORCI na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani, Crispin Kahesa amesema kila mwaka inakadiriwa Tanzania kuna wagonjwa wa saratani zaidi ya 42,060 asilimia 13 ndiyo hufika hospitali ni takriban wagonjwa 12,600.

“Hawa wanaokuja hospitalini asilimia 70 ndiyo huweza kukaa na kuendelea na tiba, asilimia 30 huwa wanakatiza au wanapotea kwa sababu tofauti tofauti ikiwamo mtazamo na hofu waliyonayo juu ya ugonjwa huo.

“Lakini pia kwa sababu huduma hizi zipo mijini zaidi, inawezekana wanapotea kwa kuwa wana majukumu mengi, watu wana changamoto nyingi za kiuchumi na kijamii,” amebainisha.

https://matukionamaisha.blogspot.com/

Makabidhiano ya mashine mpya ya X-ray(digital x-ray machine) chini ya mpango wa MES(Managed Equipment System)

      Comments Off on

Makabidhiano ya mashine mpya ya X-ray(digital x-ray machine) chini ya mpango wa MES(Managed Equipment System)

Mashine hii inauwezo wa kuingiza vipimo vyote vya x-ray hivyo kusaidia kurahisisha huduma kwa wagonjwa na huondoa usumbufu wa kusubili vipimo kwa wagonjwa, pia itaongeza ufanisi na ubora wa vipimo kwani ni ya kisasa na inatumia huduma za kisasa.Pia machine hizi zimekuja na  vifaa vya kujulinda dhidi ya mionzi kwa watumiaji wa machine pamoja na wagonjwa

Mkurugenzi pamoja na Mkurugenzi wa Tiba na wafanyakazi wa Taasisi ya saratani ya ocean Road, Pamoja na wataalamu wa mionzi(x-ray) wakiwa katika picha ya pamoja katika makabidhiano ya mashine ya X-rays chini ya mpango wa MES(Managed Equipment System)

Mkurugenzi pamoja na Mkurugenzi wa Tiba na wafanyakazi wa Taasisi ya saratani ya ocean Road katika makabidhiano ya mashine ya X-rays chini ya mpango wa MES(Managed Equipment System)

Mkurugenzi pamoja na Mkurugenzi wa Tiba na wafanyakazi wa Taasisi ya saratani ya ocean Road wakikagua vifaa(protective gown) vya kujilinda dhidi ya mionzi
Mkurugenzi pamoja na Mkurugenzi wa Tiba na wafanyakazi wa Taasisi ya saratani ya ocean Road wakionyesha stika na mtaalam wa mashine za X-ray

Mkurugenzi pamoja na Mkurugenzi wa Tiba(kushoto, akiwa amevaa nguo ya kujikinga na mionzi) na wafanyakazi wa Taasisi ya saratani ya ocean Road wakisikiliza maelekezo kutoka kwa mtalaam wa mionzi

Mkurugenzi(kulia) wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road akitoa shukrani na kuwapongeza wa Taaalamu wa mionzi(x-ray) na wafanyakazi wote wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road walioshiriki katika makabidhiano hayo ya mashine chi ya mapango wa MES

Kikao cha Baraza la wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road

      Comments Off on Kikao cha Baraza la wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road

Kikao cha kwanza cha baraza la tano la wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road kilifanyika tarehe 27/08/2020 katika ukumbi wa mikutano wa Kibaha Conference Centre. Kikao hicho kilichohudhuriwa na wajumbe wa TUGHE taifa na mkoa kilianza saa tatu kamili asubuhi kwa sala maalumu ya kuliombea baraza, Taasisi na Taifa katika utekelezaji ulio bora wa majukumu.

Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wakiwa katika picha ya pamoja

Baada ya wajumbe kujitambulisha, Mwenyekiti Ndugu. Julius Mwaiselage, aliwashukuru wajumbe kwa kuhudhuria mkutano katika muda uliopangwa na kuelezea mafanikio ya kiujumla ambayo baraza iliyapendekeza katika vikao vilivyopita na Taasisi kuyatekeleza. Miongoni mwa mafanikio hayo ni:

    Katika kikao hicho, baraza lilisikiliza na kujadili:

      Wajumbe wa baraza wakisikiliza kwa umakini uwasilishwaji wa ripoti za baraza la wafanyakazi
Wajumbe wa baraza wakisikiliza kwa umakini uwasilishwaji wa ripoti za baraza la wafanyakazi
Wajumbe wa baraza wakisikiliza kwa umakini uwasilishwaji wa ripoti za baraza la wafanyakazi
Wajumbe wa baraza wakisikiliza kwa umakini uwasilishwaji wa ripoti za baraza la wafanyakazi