Parokia ya Kibamba waishukuru ORCI kuwapelekea huduma uchunguzi wa Saratani
Waamini wa Kanisa Katoliki Mtakatifu Vincent wa Paulo, Parokia ya Kibamba, wamewashukuru wataalamu wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI), kwa kuwapeleka huduma ya uchunguzi wa afya bila malipo.
Kanisa hilo jana liliadhimisha kumbukumbu ya Mtakatifu Vincent wa Paulo ambaye ni somo wa parokia. Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya waumini wa kanisa hilo, wamesema kufikishiwa huduma hizo za uchunguzi imekuwa jambo jema kwani wamepima na kujitambua afya zao.
“Tunasherehekea kumbukumbu ya Mtakatifu Vincent wa Paulo, Baba Paroko wetu, aliona vema wataalamu waje kanisani nasi tupate huduma za uchunguzi, nimefarijika mno, nimechunguzwa saratani ya kizazi na matiti bila malipo, nimeambiwa nipo vizuri, nina amani moyoni mwangu,” alisema mmoja wa waumini hao.
Muuguzi wa Kitengo cha Uchunguzi wa Saratani ORCI, Beatrice Mushi alisema waliwachunguza jumla ya waamini 168.
“Katika idadi hiyo 81 tuliwachunguza saratani ya matiti ambapo wawili tuliwakuta na uvimbe ni kiashiria cha awali cha saratani, 59 tuliwachunguza saratani ya kizazi watatu kati yao tuliwakuta na viashiria vidogo vya saratani na mmoja kiashiria kikubwa,” alisema.
Aliongeza “Kwa upande wa saratani ya tezidume waliochunguzwa ni wanaume 28 ambapo wawili kati yao tuliwakuta na viashiria vya saratani, tuliowakuta na viashiria tumewapa rufaa kuja kule kwenye taasisi yetu kwa uchunguzi zaidi na matibabu.
Awali wakati wa ufunguzi wa maadhimisho hayo, Paroko wa Kanisa hilo, Padre Prejo Joseph aliwashukuru wataalamu wote wa afya waliokubali kujumuika nao katika maadhimisho hayo pamoja na wataalamu wa masuala ya kisheria.
Dc. Jokate ahimiza jamii kutembelea, kuwafariji wagonjwa
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegero amepokea msaada wa vifaa tiba vilivyotolewa na Jema Foundation kwa ajili ya wagonjwa wanaopatiwa matibabu ya saratani katika Taasisi ya Saratani Ocean Road.
Taasisi hiyo inasimamiwa na Jema Baruani ambaye ni miongoni mwa wagonjwa waliowahi kutibiwa saratani Ocean Road na kupona sasa akijitolea kuendelea kuelimisha jamii kuhusu magonjwa hayo.
Akipokea msaada huo, amehimiza jamii kuendeleza utamaduni wa kuwatembelea, kuwajulia hali wagonjwa waliolazwa wodini, hospitalini walimolazwa ili kupatiwa matibabu dhidi ya maradhi mbalimbali yanayowakabili.
“Hakuna anayeijua kesho yake,” amesisitiza.
Dc jokate ametumia mfano hai wa shangazi yake ambaye alijiwekea utaratibu wa kuwatembelea na kuwasaidia wagonjwa pasipo kujua kwamba kitendo hicho siku moja kingekuwa msaada mkubwa kwake.
“Alikuwa anajitoa sana, kila alipotoka kazini aliwatembelea wagonjwa wa saratani, sasa hivi ni mstaafu, wakati alipokuwa anafanya vile hakuwahi kufikiri siku moja itakuwa sehemu muhimu ya kipenzi chake (mume wake), kwenda kutibiwa.
“Kwa hiyo, alipolazwa kwa matibabu, kwa kuwa yeye (shangazi) alikuwa tayari anafahamika, ilikuwa wepesi kusaidiwa pia. Tunayoyafanya sasa ni hazina ya maisha yetu ya baadae,” amesisitiza.
Amewapongeza Jema Foundation kwa kujitoa kwa jamii hususan wagonjwa wa saratani kwa kuwatembelea na kuwafariji kila mwaka.
“Nawapongeza madaktari na wataalamu wote wa Ocean Road kwa kazi kubwa wanayofanya ya kuwahudumia wagonjwa hawa,” amesema.
Ameongeza “Kipekee naipongeza Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, imesimika vifaa vya kisasa hapa Ocean Road na sasa tunashuhudia inapokea wagonjwa wengine pia kutoka nje ya Tanzania.
“Daktari (Crispin Kahesa), amenieleza kwamba wanapokea wagonjwa kutoka nje ya nchi kwa sababu kuna uwezekaji mkubwa umefanywa na Serikali kwa kusimika mashine ambazo wenzetu kwenye nchi zao hawana.
“Amenieleza, huduma za tiba ya saratani zinayopatikana Tanzania ni bora za viwango vya kimataifa na gharama ni nafuu kulinganisha na mataifa mengine.
“Haya ni mambo ambayo lazima tuwaambie Watanzania, wajue kwamba tuna vitu ambavyo wengine wanatamani kuwa navyo, waje wapatiwe huduma bora,” ametoa rai Mkuu huyo wa Wilaya.
Mwakilishi wa Jema Foundation, Jema Baruani amesema wagonjwa wengi wa saratani huwa na hofu pale wanapogundulika, wapo wengine ambao huacha matibabu.
“Si wote huwa na moyo wa ujasiri kama mimi, wapo wanaokata tamaa, si wote wana uwezo wa kulikabili gonjwa hili, inabidi sisi ambao Mungu ametujalia, tujitoe katika hali na mali, kuwaona… unaweza ukaja hapa japo kuwaambia neno pole, ikawa ahueni kwao,” amesema.
Jema ametoa rai pia kwa jamii hususan vijana kuwa na ujasiri na kujitokeza kufanyiwa uchunguzi wa saratani kwani ikiwa kugundulika, mtu hupona baada ya matibabu.
Mkurugenzi wa Kinga wa ORCI na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani, Crispin Kahesa amesema kila mwaka inakadiriwa Tanzania kuna wagonjwa wa saratani zaidi ya 42,060 asilimia 13 ndiyo hufika hospitali ni takriban wagonjwa 12,600.
“Hawa wanaokuja hospitalini asilimia 70 ndiyo huweza kukaa na kuendelea na tiba, asilimia 30 huwa wanakatiza au wanapotea kwa sababu tofauti tofauti ikiwamo mtazamo na hofu waliyonayo juu ya ugonjwa huo.
“Lakini pia kwa sababu huduma hizi zipo mijini zaidi, inawezekana wanapotea kwa kuwa wana majukumu mengi, watu wana changamoto nyingi za kiuchumi na kijamii,” amebainisha.
Makabidhiano ya mashine mpya ya X-ray(digital x-ray machine) chini ya mpango wa MES(Managed Equipment System)
Mashine hii inauwezo wa kuingiza vipimo vyote vya x-ray hivyo kusaidia kurahisisha huduma kwa wagonjwa na huondoa usumbufu wa kusubili vipimo kwa wagonjwa, pia itaongeza ufanisi na ubora wa vipimo kwani ni ya kisasa na inatumia huduma za kisasa.Pia machine hizi zimekuja na vifaa vya kujulinda dhidi ya mionzi kwa watumiaji wa machine pamoja na wagonjwa
Mkurugenzi pamoja na Mkurugenzi wa Tiba na wafanyakazi wa Taasisi ya saratani ya ocean Road, Pamoja na wataalamu wa mionzi(x-ray) wakiwa katika picha ya pamoja katika makabidhiano ya mashine ya X-rays chini ya mpango wa MES(Managed Equipment System)
Mkurugenzi pamoja na Mkurugenzi wa Tiba na wafanyakazi wa Taasisi ya saratani ya ocean Road katika makabidhiano ya mashine ya X-rays chini ya mpango wa MES(Managed Equipment System)
Mkurugenzi pamoja na Mkurugenzi wa Tiba na wafanyakazi wa Taasisi ya saratani ya ocean Road wakikagua vifaa(protective gown) vya kujilinda dhidi ya mionzi
Mkurugenzi pamoja na Mkurugenzi wa Tiba na wafanyakazi wa Taasisi ya saratani ya ocean Road wakionyesha stika na mtaalam wa mashine za X-ray
Mkurugenzi pamoja na Mkurugenzi wa Tiba(kushoto, akiwa amevaa nguo ya kujikinga na mionzi) na wafanyakazi wa Taasisi ya saratani ya ocean Road wakisikiliza maelekezo kutoka kwa mtalaam wa mionzi
Mkurugenzi(kulia) wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road akitoa shukrani na kuwapongeza wa Taaalamu wa mionzi(x-ray) na wafanyakazi wote wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road walioshiriki katika makabidhiano hayo ya mashine chi ya mapango wa MES
Comments Off on Kikao cha Baraza la wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road
Kikao cha kwanza cha baraza la tano la wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road kilifanyika tarehe 27/08/2020 katika ukumbi wa mikutano wa Kibaha Conference Centre. Kikao hicho kilichohudhuriwa na wajumbe wa TUGHE taifa na mkoa kilianza saa tatu kamili asubuhi kwa sala maalumu ya kuliombea baraza, Taasisi na Taifa katika utekelezaji ulio bora wa majukumu.
Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wakiwa katika picha ya pamoja
Baada ya wajumbe kujitambulisha, Mwenyekiti Ndugu. Julius Mwaiselage, aliwashukuru wajumbe kwa kuhudhuria mkutano katika muda uliopangwa na kuelezea mafanikio ya kiujumla ambayo baraza iliyapendekeza katika vikao vilivyopita na Taasisi kuyatekeleza. Miongoni mwa mafanikio hayo ni:
Katika kikao hicho, baraza lilisikiliza na kujadili:
Wajumbe wa baraza wakisikiliza kwa umakini uwasilishwaji wa ripoti za baraza la wafanyakazi
Wajumbe wa baraza wakisikiliza kwa umakini uwasilishwaji wa ripoti za baraza la wafanyakazi
Wajumbe wa baraza wakisikiliza kwa umakini uwasilishwaji wa ripoti za baraza la wafanyakazi
Wajumbe wa baraza wakisikiliza kwa umakini uwasilishwaji wa ripoti za baraza la wafanyakazi
Comments Off on UWASILISHAJI WA RIPOTI YA QIT NA UGAWAJI WA ZAWADI KWA WASHINDI
Siku
ya Ijumaa tarehe 14/08/2020 kupitiakwenyekipindi cha elimuendelevu ya matibabu
(CME), ndugu Hemed Myanza, mjumbe wa timu ya kuboresha huduma ya Taasisi ya
Saratani Ocean Road, aliwasilisharipoti ya utekelezaji wa majukumu ya kamati ya
kuboresha huduma (QIT) kwa mwaka 2019.
Muwasilishaji
wa madandugu Hemed Myanza
Ripotihiyoiliangaziahalihalisi
ya ORCI kabla ya kuanza utekelezaji wa nadharia ya 5S KAIZEN TQM na baada ya
kuanza utekelezaji, changamoto, mafanikio, mapendekezo na uchanganuzi wa
uboreshwaji wa huduma ndani ya kipindihicho.
MkurugenziMtendaji
wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (katikati), akiwa na Mwenyekiti wa QIT Albina Kirango (Kushoto) na Katibu wa
QIT Mohamed Mbwana (Kulia)
Wafanyakazi
wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, wakisikilizaripoti ya utekelezaji wa
majukumu ya QIT kwa mwaka 2019
Wafanyakazi
wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, wakisikilizaripoti ya utekelezaji wa
majukumu ya QIT kwa mwaka 2019
Wafanyakazi
wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, wakisikilizaripoti ya utekelezaji wa
majukumu ya QIT kwa mwaka 2019
Wafanyakazi
wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, wakisikilizaripoti ya utekelezaji wa
majukumu ya QIT kwa mwaka 2019
Baada
ya wasilisho la ripoti, Zawadi zilikabidhiwa kwa
vitengovilivyofanyavizurikatikautekelezaji wa uboreshaji wa huduma
kupitianadharia ya 5S KAIZEN TQM, ambapowashindiwalikuwakamaifuatavyo:
Mshindi
wa kwanza: Kitengo cha Famasia – OCP
Mkurugenzimtendajiakiwakatikapicha
ya pamoja na washindi kutoka Famasia OCP
Mshindi
wa Kwanza: Kitengo cha Maabara – General
Watumishi
wa maabara – general wakinyanyuajuukikombe cha ushindi
Mshindi
wa Pili: Kitengo cha Famasia – General
Washindi
kutoka Famasia general, wakikabidhiwacheti cha ushindi na mkurugenziMtendaji
Mshindi
wa tatu: Kitengo cha Maabara – Bima
Washindi
kutoka maabarabima, wakiwakatikapicha ya pamoja na MkurugenziMtendaji
Washindiwalikabidhiwa
Zawadi ya vikombe, ambavyovilitolewa na Mkurugenzimtendaji wa Taasisi ya
Saratani Ocean Road, ndugu Julius Mwaiselage. Mkurugenzialiwapongezawashindi na
kuwahimizawatumishi wote katikavitengovilivyoshiriki, kuhakikishakuwa,
wakatiujaonaowanafanyavyema zaidi. Kwanidhima ta kuboresha huduma ni
sualamtambuka na linalopaswakutekelezwavyemasehemu zote za kutolea huduma.
Mkurugenzialiwapongezawanatimu wa QIT na kuwataka kuendeleza na utekelezaji wa
majukumu yao, ikiwamo na kuongeza kufanya tafitijuu ya hali ya kuridhika kwa
huduma kwa wateja wa Taasisi
Glioblastoma
ni miongoni mwa aina za Saratani zinazoushambulia ubongo wa mgonjwa. National
Glioblastoma awareness day huadhimishwa kila mwaka duniani tarehe 22/07/2020.
Katika maadhimisho ya siku hiyo Dr Mark Mseti alitoa mada katika ukumbi wa
mikutano wa Mwalimu Nyerere Conference uliopo katika Taasisi ya Saratani Ocean
Road kuhusu Glioblastoma.
Wafanyakazi
wa Taasisi ya Saratani Ocean Road wakimsikiliza Mtoa Mada (Dr Mseti) katika
maadhimisho ya siku ya Glioblastoma duniani
Wafanyakazi
wa Taasisi ya Saratani Ocean Road wakimsikiliza Mtoa Mada (Dr Mseti) katika
maadhimisho ya siku ya Glioblastoma duniani
Wafanyakazi
na wanafunzi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road wakimsikiliza Mtoa Mada (Dr
Mseti) katika maadhimisho ya siku ya Glioblastoma duniani
Wafanyakazi
wa Taasisi ya Saratani Ocean Road wakimsikiliza Mtoa Mada (Dr Mseti) katika
maadhimisho ya siku ya Glioblastoma duniani
Wanafunzi na
washiriki wengine wakimsikiliza Mtoa Mada (Dr Mseti) katika maadhimisho ya siku
ya Glioblastoma duniani
Glioblastoma
ndio aina ya saratani ya ubongo inayosumbua zaidi duniani. Ugonjwa huo ndio
ulioondoa maisha ya mwanasiasa maarufu marekani Hayati Sen. John McCainn. Elimu
hii imedhaminiwa na Hetero Biopharma watengenezaji was dawa mbalimbali za
saratani.
Mtoa
maada akipokea tuzo kutoka kwa Mfamasia Mkuu wa Taasisi huku akishuhudiwa na Bw
Jawan kutoka Hetero Biopharma.