ORCI YAANZISHA HUDUMA YA KUTUMIA MIONZI YA IMRT

      Comments Off on ORCI YAANZISHA HUDUMA YA KUTUMIA MIONZI YA IMRT

TAASISI ya  Saratani ya Ocean Road (ORCI) imeanzisha huduma mpya ya kibingwa ya kutibu ugonjwa wa saratani kwa miale ya mionzi kwa njia ya  kisasa zaidi ijulikanayo kama Intensity  Modulated Radiation Therapy (IMRT), ambapo tiba yake ni ya mionzi ikiwa inatibu  eneo mahususi  yenye tatizo pekee.

Tanzania inakuwa ya kwanza kutumia huduma hiyo ya IMRT kwa ukanda huu wa Afrika  Mashariki huku kwa Afrika inaingia kuwa nchi ya tatu baada ya Afrika Kusini na Misri.

Kwa mataifa mengine huduma hiyo inatolewa kwa nchi za Marekani na India pamoja na baadhi ya nchi ya za Ulaya.

Akizungumza na waandishi wa Habari, Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dk. Julius Mwaiselage, alisema kwa sasa wagonjwa waliokuwa wakienda kutibiwa Nchini  India watakaporejea wataweza kutibiwa hapahapa kwa sasa kwani tayari wamenzisha huduma hiyo.

‘Huduma hii awali ilikuwa inapatikana nje ya nchi haswa nchi zilizoendelea ikiwe, India. Hivyo hata wagonjwa watakaporejea  hapa nchini wataweza kupata tiba hii hapa hapa  na wakaendelea na matibabu.

“Awali tulikuwa tunatoa tiba ya teknolojia ya 3D ambapo kwa sasa tumeziongezea uwezo yaani kuzimobireti na kuja na huduma hii mpya kwa kutumia mashine hizi hizi za ‘LINAC ACCELERATOR.’ Alisema Mwaiselage.

Dk. Mwaiselage amesema mashine hizo zimenunuliwa  kwa fedha za Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dk. John Pombe Joseph  Magufuli zikiwa mpya kabisa kutoka kiwandani kwa TSh. bilioni 9.5  zikiwa mbili  ya mionzi na ya kupanga tiba, mwaka 2018 na kuzinduliwa rasmi na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan mwaka 2019 ambapo imekuwa na uwezo wa kutoa  tiba mbalimbali za mionzi ikiwemo teknolojia ya 3D na zingine zikiwemo ya tiba ya upasuaji wa mionzi na zinginezo.

‘Toka zimefka hizi mashine tulianza na hii ya mionzi kwa teknolojia  ya 3D, lakini kwa sasa mashine hizi tumezi ongezea  uwezo ‘upgrade’  na  kuanza kutumia tiba hiyo ya kisasa zaidi ya IRMT ambayo kwa sasa inatumika Duniani kote ikiwemo Afrika Kusini, Lakini India na Marekani.

Tiba hii ni mahususi kabisa kwa kutibu maeneo yale ambayo ungeona hauitaji kufikiwa n miale ya mionzi mikali kwenye eneo ambalo usingetaka iguswe.

Kwa upande wake Daktari bingwa wa Saratani wa ORCI, Dk.Sikudhani  Muya alisema kuwa tiba hii mpya ni maalum ambapo itasaidia kuzuia mionzi mikali kuzuiwa isipenye maeneo mengine isidhurike.

‘Huduma hii inasaidia kutibu eneo lenye saratani  kwa miale yake ya mionzi kuenda kutibu eneo lile pekee lenye tatizo. Mfano  uvimbe wa saratani ukiwa eneo la kichwa basi tiba hii mionzi yake itaenda kutibu tu eneo hilo na sehemu za ubongo hazitaguswa. 

Hii ndio faida kuu ya tiba hii na ni ya kipekee sana ambapo inachukua dakika kuanzia 10 hadi 30.’ Alisema Dk. Muya.

HUDUMA ZA MAMMOGRAPHY

      Comments Off on HUDUMA ZA MAMMOGRAPHY

Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, inapenda kuwaarifu wananchi wa Tanzania kuwa, huduma za kisasa za uchunguzi wa Saratani ya matiti kwa machine ya mammogram imerejea.

Uchunguzi kwa kutumia mammography ni njia mahsusi ya upimaji wa titi unaotumia dozi ndogo ya X RAY kutambua uwepo wa saratani mapema kaba ya mwanamama hajaanza kuonesha dalili nyengine. Uchunguzi huu huwa ni wa mapema na husaidia Zaidi katika kutibu saratani ya matiti.

UJUMBE KUTOKA BURUNDI WATEMBELEA TAASISI YA SARATANI KWA AJILI YA MAFUNZO

      Comments Off on UJUMBE KUTOKA BURUNDI WATEMBELEA TAASISI YA SARATANI KWA AJILI YA MAFUNZO

Ujumbe wa wataalamu watano wakiwemo Madaktari na maafisa kutoka Wizara ya Afya ya Burundi upo nchini kwa ziara maalumu ya siku tano kujifunza mambo mbalimbali ya utendaji na uendeshaji unaofanywa na Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) ikiwemo namna inavyotoa huduma zake za matibabu kwa wagonjwa wa Saratani kwa ubora Ukanda wa Afrika Mashariki.

Ujumbe huu maalumu, unalenga kuitumia safari hii ya mazfunzo kwa ajili ya kuja kuanzisha hospitali kama ya Ocean Road pindipo wakirejea nchini Burundi.

Awali akizungumza na wanahabari, Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dkt. Julius Mwaiselage amesema wameupokea ujumbe huo kutoka Burundi na utakuwa nchini kwa siku tano kujifunza ili kupata uzoefu ambapo nao wakiwa mbioni kuanzisha huduma kama hizo nchini mwao. Wataalamu hao, walikaribishwa na mwenyeji wao, Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dr Julius Mwaiselage, ambaye aliwakaribisha na kuwaeleza kuwa Taasisi kama wawakilishi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, wana fahari kubwa kuwa wakufunzi wa timu hiyo kutoka Burundi, na kuwa wataalamu wa Taasisi watatumia muda huo wa siku tano kuweza kuwafunza masuala mtambuka yatakayowawezesha na wao wakirudi kwao waweze kuanzisha huduma za matibabu ya saratani.

Mkurugenzi aliwaarifu kuwa, tayari kuna programu za mafunzo ya madaktari na wataalamu wa onkolojia inayoendeshwa kwa kushirikiana na chuo kikuu cha tiba cha MUHAS. Hivyo watumie fursa hiyo kuwaleta wanafunzi kuja kujiunga na programu hizo

Ugeni huo pia utapata nafasi ya kujifunza kwa nadharia na vitendo ambapo watazunguka katika kujionea jinsi huduma zinavyotolewa na namna wanavyoendesha matibabu ikiwemo kutumia mitambo ya kisasa inayotumia miale ya mionzi, mashine ya Linac Accelerator inayopatikana Tanzania pekee katika Ukanda wa Afrika Mashariki.

 “Kama inavyofahamika ukanda huu wa Afrika hususani Tanzania, ORCI imepiga hatua kubwa sana katika utoaji wa huduma za saratani kwa wananchi wake.

“Hivyo Shirika la IAEA limeona ni busara sana kwa zile nchi ambazo zinataka kuanzisha huduma zake za saratani, zifike Tanzania hapa kwetu ili kujifunza mambo mbalimbali ambayo yamefanyika kwa weredi na kwa upana mkubwa mno,” amesema.

Ameongeza “Ujumbe huu utajifunza pia  tulivyofanya kwa kupitia uboreshaji wa huduma kutibu saratani kwenye vituo, uboreshaji wa tiba  ya kutibu kwenye Kanda, na uboreshaji wa Ocean road kupitia kununua mashine mpya.

“Pia uboreshaji wa tiba kemia, upatikanaji wa dawa pamoja na mafunzo kwa watumishi wa Afya katika utoaji wa huduma ya saratani,” amesema Dk. Mwaiselage.

Amesema sasa wanatarajia kuendelea kupokea ugeni mwingine kama huo kutoka nchi mbalimbali zikiwemo za Liberia na Lesotho amabazo zitafika nchini kujifunza juu ya utoaji na tin ya Saratani.

Dk. Mwaiselage ameipongeza Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais John Magufuli kwa kuwezesha taasisi hiyo kiasi kwa sasa imekuwa kimbilio kwa nchi nyingi ambazo zinataka kuja kujifunza namna ya tiba ya Saratani.

“Kwa kipindi hiki cha miaka minne taasisi imekuwa mbele sana katika utoaji wa huduma na nchi nyingi imeona Tanzania tukipiga hatua kwenye kutibu saratani ikiwemo kununua mashine hizi mionzi za kisasa za LINAC ambazo zinapatikana katika nchi chache sana za Afrika huku zikipatikana nchi chache za Ulaya, India na Marekani,” amesema.

Amesema wamejitahidi katika upatikanaji wa dawa za saratani ambazo zinapatikana kwa kiwango kikubwa sana na wagonjwa wanatibiwa vizuri.

3 STAR SLIPTA LABORTAORY AWARD FOR ORCI

      Comments Off on 3 STAR SLIPTA LABORTAORY AWARD FOR ORCI

SLIPTA is a framework for improving quality of public health laboratories in developing countries to achieve the requirements of the ISO 15189 standard. It is a process that enables laboratories to develop and document their ability to detect, identify, and promptly report all diseases of public health significance that may be present in clinical specimens.

This initiative was spearheaded by a number of critical resolutions, including Resolution AFR/RC58/R2 on Public Health Laboratory Strengthening, adopted by the Member States during the 58th session of the Regional Committee in September 2008 in Yaoundé, Cameroon, and the Maputo Declaration to strengthen laboratory systems

This quality improvement process towards accreditation further provides a learning opportunity and pathway for continuous improvement, a mechanism for identifying resource and training needs, a measure of progress, and a link to the WHO/AFRO National Health Laboratory Service Networks.

Recently, on the concluded SLIPTA audit at Ocean Road Cancer Institute Laboratories, the institute was awarded a 3 star after scoring 203/273 equivalent to 76.2%. This is to acknowledge the ability of the Ocean Road Cancer Institute to comply with the quality standard set by the WHO.

ORCI Celebrates 2020 International women’s day

      Comments Off on ORCI Celebrates 2020 International women’s day

International women’s day is celebrated on 8th of March each year. In 2020 the world celebrated with a theme of equality for all.

International Women’s Day 2020 campaign theme is #EachforEqual.  An equal world is an enabled world.  Individually, we’re all responsible for our own thoughts and actions – all day, every day. We can actively choose to challenge stereotypes, fight bias, broaden perceptions, improve situations and celebrate women’s achievements. Collectively, each one of us can help create a gender equal world

During the 2020 celebration which was held in leaders club, Dar es Salaam, Tanzania, ORCI staff turned out in number to participate the event and loudly spread the message on how women at ORCI jointly utilize their skills, experience and expertise in providing general cancer care and management.

We wish all women in the world, a happy women’s day.

Uzinduzi wa Muongozo wa Tiba ya Saratani nchini Tanzania na Tamko la Waziri afya katika Siku ya Saratani Duniani

      Comments Off on Uzinduzi wa Muongozo wa Tiba ya Saratani nchini Tanzania na Tamko la Waziri afya katika Siku ya Saratani Duniani

Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb) mnamo tarehe 03/02/2019 katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere katika Hospitali ya Saratani ya Ocean Road , akiwa ni mgeni rasmi, alizindua rasmi muongozo wa taifa wa tiba ya saratani na kutumia fursa hiyo kutoa tamko la Serikali katika maadhimisho ya siku ya Saratani duniani yanayofanyika Tarehe 4 Februari ya kila mwaka. Mheshimiwa Ummy Mwalimu, alieleza kuwa kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni “Mimi na Nitafanya”.

Pia, alishajihisha Taasisi ya Saratani ya Ocean Road kuendeleza na kutoa elimu za visababishi, dalili za kutambua saratani na kile kinachopaswa kufanyika pale ambapo tayari Mwananchi anapokuwa amegundulika na ugonjwa wa Saratani. Aliitaka Taasisi ya Saratani Kuendelea kutoa mtazamo chanya na kujikita Zaidi katika kutoa huduma bora kama zinavyoelekezwa katika muongozo unaozinduliwa.

Waziri Ummy Mwalimu alizindua muongozo huo na kutoa takwimu za ukubwa wa tatizo la saratani duniani na hapa nchini, huku akipongeza juhudi zilizopo nchini Tanzania za kuongeza hospitali za kutibu wananchi dhidi ya ugonjwa wa Saratani. Takwimu zinaonyesha kuwa katika kila watu 100,000 kuna wagonjwa 76 wapya wa saratani. Huku vifo vinavyosababishwa na ugonjwa huo kufikia 68 kwa kila wagonjwa 100. Hali hii ya vifo inatokana hasa na wagonjwa wengi kuhudhuria hospitali wakiwa katika steji ya mwisho.

Waziri Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Muongozo wa Taifa katika kutoa tiba ya Saratani

Waziri aliwashukuru wadau walioshiriki katika kufanikisha kuandaa mpango huo wa taifa wa tiba ya saratani na kuwataka wanahabari kubeba jukumu la kuelimisha wananchi, ili kuongeza idadi ya wananchi wanaoenda hospitali kufanya uchunguzi na hivyo kugundua tatizo mapema na kuongeza idadi ya wanaotibiwa na kupona.

Waziri Ummy aligawa nakala za muongoz huo wa Taifa kwa wakurugenzi na wawakilishi wa wakurugenzi wa hospitali zinazotoa matibabu ya ugobjwa wa saratani nchini ikiwemo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, MOI, Bugando na KCMC. Pia aligawa nakala za vyeti vya shukrani kwa wadau waliochangia kufanyika kwa kazi ya kuandaa muongozo huo wa kitaifa. Wadau hao ni Pamoja na American Cancer Society, Roche pharmaceutical Tanzania, HeteroBiopharama LTD na University of California San Fransisco,

Waziri Ummy Mwalimu akimkabidhi cheti cha shukran mwakilishi wa University of California San Fransisco

Awali Akimkaribisha mgeni rasmi, kuhutubia na kuzindua muongozo huo wa taifa, Dr Grace Maghembe alimueleza Mheshimiwa Waziri kuwa Saratani bado ni miongoni mwa magonjwa yanayoongoza duniani kwa kusababisha vifo kwa watu wengi. Dr Maghembe alieleza kuwa, kutokana na takwimu hizo, na kwa kuwa tayari huduma za kutibu ugonjwa wa Saratani nchini Tanzania zimeongezeka kwa hospitali nyingi Zaidi kutoa huduma hizo, Wizara kwa kushirikiana na Taasisi ya Saratani ya Ocean Road na wadau wengine wa afya, waliandaa timu ya Pamoja ya kuandaa mpango wa taifa wa kusimamia utoaji wa huduma za Saratani.

Dr Maghembe alisema kuwa muongozo huo unatoa maelekezo na majukumu ya kila ngazi ya hospitali kutoka zahanati mpaka kufikia hospitali bingwa na za rufaa. Kwa kiasi kikubwa, muongozo umezingatia sana kinga, kwani kinga ni bora kuliko tiba. Hivyo uchunguzi wa mapema wa kila aina ya saratani umezingatiwa na umeelezwa kwa kina katika muongozo huo.

Nae, Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, alieleza kwa kina namna ambavyo Taasisi ya Saratani ya Ocean Road imejiimarisha na kuboresha huduma zake kuanzia 2015. Mkurugenzi huyo alieleza kazi kubwa iliyofanywa na wafanyakazi wa Ocean Road na timu iliyoteuliwa katika kuandaa muongozo huo na kuwanasihi sana wataalamu wa hospitali zote zinazotoa matibabuu ya saratani nchini kuzingatia kwa kina yaliyoelezwa kwenye muongozo huo. Pia alitumia fursa hiyo, kuwaeleza wananchi kwa ujumla kuwa, Taasisi ya Saratani ya Ocean Road katika wiki hii ya maadhimisho ya Ugonjwa wa Saratani duniani, kuwa itaendelea na kutekeleza majukumu yake ya kufanya zoezi la uchunguzi wa awali wa magonjwa ya saratani.

Mkurugenzi aliwashukuru sana, wadau wote walioshirikiana na Wizara ya Afya na Taasisi ya Ocean Road katika kuandaa muongozo huo.

Uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi

      Comments Off on Uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi

Baraza la tano la wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road lilizinduliwa tarehe 28/1/2020 katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu. Nyerere uliopo katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road. Kabla ya kuzinduliwa kwa baraza hilo ulifanyika uchaguzi wa katibu na katibu msaidizi wa Baraza ambapo ndugu Yusuph Fikirini alichaguliwa kuwa katibu na ndugu Joha Kibira kuwa Katibu Msaidizi.

Picha ya pamoja Mgeni Rasmi na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi – ORCI

Picha Mwenyekiti akiwaongoza wajumbe katika uchaguzi wa Katibu wa Baraza

Mwenyekiti akiwatambulisha Katibu na Katibu msaidizi wa Baraza mara baada ya kuchaguliwa.

Mgeni rasmi akishiri kuimba wimbo wa mshikamano daima alipowasili ukumbini

Katibu wa Baraza akitoa utambulisho wa wajumbe wanaounda Baraza kwa Mgeni rasmi

Kabla ya uzinduzi Mwenyekiti wa Baraza ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dr. Julius Mwaiselage, alitoa taarifa ya utendaji ya Taasisi na Baraza lililomaliza muda wake. Kuwa, baraza lilitekeleza wajibu wake kwa kuibua na kujadiliana njia za kuoberesha huduma za Taasisi Pamoja na kuipitia maoteo ya bajeti ili kupata mahitaji halisi ya Taasisi kutoka kila idara.

Mwenyekiti wa Baraza akito hotuba ya utangulizi kabla ya uzinduzi wa Baraza.

Baraza hili lilizinduliwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mheshimiwa Dkt. Zainabu Chaula.

Akizindua Baraza Katibu Mkuu katika hotuba yake aliwaagiza na kuwataka wafanyakazi kwa kupitia wajumbe wa baraza kukuhakikisha yafuatayo;

  • Wafanyakazi wawe huru kushauri na Viongozi wakubali kushauriwa
  • Kuzidi kuboresha wamasiliano
  • Kuendelea kutoa huduma bora kwa wagonjwa ikiwa ni pamoja na kuwahurumia na kuwafariji,
  • Kuepuka vitendo vya rushwa
  • Wawakilishi wa baraza wasaidie kuwabadilisha wafanyakazi wengine waweze kufanyakazi vizuri ili kwa pamoja tuweze kutimiza adhi ya Serikali ya Kuboresha afya za wananchi.

Wajumbe wa Baraza wakifiatilia hotuba ya Mgeni Rasmi

Baada ya uzinduzi wajumbe wa baraza walipata mafunzo juu ya uendeshaji wa mabaraza, Utawala bora na mapambano dhidi ya rushwa mahali pa kazi.

Mwezeshaji akiendelea kuwasilisha mada ya uendeshaji wa mabaraza

Wajumbe wakifuatilia mada inayowasilishwa

Announcement of the first annual nuclear science technology conference and exhibitions

      Comments Off on Announcement of the first annual nuclear science technology conference and exhibitions

TANZANIA ATOMIC ENERGY COMMISSION

ANNOUNCEMENT OF THE FIRST ANNUAL NUCLEAR SCIENCE, TECHNOLOGY CONFERENCE AND EXHIBITIONS
DATES: 19 – 21 FEBRUARY 2020

VENUE: ARUSHA INTERNATIONAL CONFERENCE CENTER (AICC) ARUSHA 

CALL FOR ABSTRACTS AND EXHIBITIONS

Announcement of the first annual nuclear science technology conference and exhibitions Read More…

ORCI doctor among recipient of Fogarty award for early career researchers

      Comments Off on ORCI doctor among recipient of Fogarty award for early career researchers

Dr. Salum Juma Lidenge a medical specialist from Ocean Road Cancer Institute, current undertaking PhD studies in the University of Nebraska-Lincon, has been named among the recipient of the Fogarty award for early career researchers. The project title is Plasma and Cellular Immune Biomarkers of Kaposi’s Sarcoma in HIV-1 Suppressed Patients (Tanzania). The objective of this proposal is to recruit Tanzanian HIV-1 PVL suppressed patients presenting with KS at ORCI, and age and sex-matched co- infected but asymptomatic controls from nearby CTCs in order to define immune responses and metabolomic profiles that differentiate the two groups. The proposed study has potential to identify biomarkers for KS diagnostics, treatment management, or to identify potential immunotherapeutic or vaccine development strategies.

Dr. Salum Juma Lidenge (left) while attending the U-54 conference in Dar es Salaam

Online statement from Fogarty international center read:

The grants will help ensure that advanced postdoctoral scientists and junior faculty have a pathway to independence, with protected time for research activities under the guidance of experienced mentors in developing countries and in the U.S”.

Recipients of 14 Emerging Global Leader Awards hold junior faculty positions and research scientist appointments at institutions in Bangladesh and India, and across Africa – in Ghana, Mali, Nigeria, South Africa and Tanzania.

The programs fund research relevant to the health priorities of the host countries, covering all health-related disciplines. Projects addressing women’s health will explore perinatal depression in adolescents, hypertension during pregnancy and improving cervical cancer detection. Many will be exploring solutions in the field of HIV and related infections, for instance working to better understand and treat HIV-related pain, identify biomarkers for Kaposi’s sarcoma, reduce HIV transmission for young women, improve home-based ART interventions and explore treatments for HIV-associated Multicentric Castleman disease. They will also study treatments for HIV-associated tuberculous meningitis, detection of multidrug-resistant TB, interactions between antiretroviral and tuberculosis drugs, and sex differences in immune response and risk for developing TB.

The new investigators will be researching chronic conditions, such as locally relevant innovations in cardiovascular disease care, and treatments for Burkitt lymphoma and building a mobile application to help detect lung cancer. Some grantees will look into issues unique to their regions, countries and communities: sickle cell disease in infants, the role of genetics in craniofacial and dental anomalies, treatment for Guillain-Barré syndrome, and causes of Shigella flexneri infections.

Partners from across NIH are supporting the Center’s career development programs. Funding for the new awards was provided by the National Cancer Institute (NCI), National Institute on Dental and Craniofacial Research (NIDCR), National Institute of Mental Health (NIMH), National Institute of Neurological Disorders and Stroke (NINDS) and NIH Office of Research on Women’s Health (ORWH). Also participating in the related funding announcements are the National Human Genome Research Institute (NHGRI) and National Institute of Environmental Health Sciences (NIEHS).

Both programs are open for future applications, with upcoming deadlines for Emerging Global Leaders on November 7 and for IRSDA on March 6.

The management of Ocean Road Cancer Institute congratulates Dr. Salum Juma Lidenge for the achievement and wishes him a successful journey in the implementation of the project ahead and would like to encourage other staff to apply for similar initiative.