TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD MAPEMA LEO IMEPOKEA TUZO YA HESHIMA YA KUTAMBUA MCHANGO WAKE KATIKA KUONA NAMNA GANI IMESHIRIKI KWENYE KUTOA ELIMU…

      Comments Off on

TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD MAPEMA LEO IMEPOKEA TUZO YA HESHIMA YA KUTAMBUA MCHANGO WAKE KATIKA KUONA NAMNA GANI IMESHIRIKI KWENYE KUTOA ELIMU…

Taasisi ya Saratani Ocean Road mapema leo imepokea tuzo ya heshima ya kutambua mchango wake katika kuona namna gani imeshiriki kwenye kutoa elimu, kufanya uchunguzi pamoja na matibabu ya magonjwa hayo.

Tuzo hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba wa Wizara ya Afya Prof. Paschal Rugajo wakati wa mkutano wa kimataifa wa kisayansi wa magonjwa yasiyoambukiza unaofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Julius Nyerere.

Akizungumza wakati wa maonesho hayo leo mchana, Prof. Rugajo amesema kuwa katika kipindi hiki Taasisi ya Saratani Ocean Road imekuwa ikifanya vizuri sana kwenye utoaji wa tiba na hii imepelekea kuaminika na mataifa ya jirani na kupelekea kupata wateja wengi kutoka nje wakihitaji kuja kutibiwa hapa katika Taasisi hiyo.

Akisisitiza Prof. Rugajo
Amesema utoaji wa huduma bora ni chachu kubwa ya tiba utalii, na ndio kitu pekee ambacho kwa sasa Tanzania inaendelea kukitilia mkazo ili kuweza kupata matokeo chanya hususan kwenye sekta hii ya Afya.

Maonesho haya yatafanyika kuanzia leo tarehe 01/11/2023 mpaka siku ya Ijumaa tarehe 03/11/2023 katika kukuza ufahamu juu ya magonjwa haya yasiyoambukizwa kwa wananchi.

UCHUNGUZI WA MAPEMA WA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI PAMOJA NA CHANJO YA PAPILLOMA VIRUS ITASAIDIA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI

      Comments Off on

UCHUNGUZI WA MAPEMA WA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI PAMOJA NA CHANJO YA PAPILLOMA VIRUS ITASAIDIA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI

“Uchunguzi wa mapema wa Saratani ya mlango wa kizazi pamoja na chanjo ya papilloma virus itasaidia katika mapambano dhidi ya Saratani ya mlango wa kizazi”.

Hayo yamesemwa na mtaalamu kutoka University of Calfornia, San Diego Dkt. Chiku Nwachukwu leo wakati anawasilisha mada inayozungumzia mionzi Tiba ya ndani kwa njia ya kisasa kwa Saratani ya mlango wa kizazi ( 3D Brachytherapy In Cervical Cancer).

Dkt. Nwachukwu amefafanua namna njia hiyo ya kisasa inavyoweza kuleta matokeo Bora zaidi katika matibabu hayo ya Saratani ya mlango wa kizazi.

Kwa upande wa waliohudhuria katika mafunzo hayo, wamepata fursa ya kuuliza maswali mbalimbali kuhusiana na tiba hiyo ya kitaalam ambapo kila mmoja slipata majibu kutoka kwa wataalam mbalimbali wa tiba hiyo waliojitokeza.

Ikumbukwe kuwa Taasisi ya Saratani Ocean Road imekwisha anza kutoa huduma ya mionzi tiba ya ndani kwa njia ya kisasa kuanzia mnamo mwezi wa Tano mwaka 2023.

KILELE CHA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KISAYANSI WA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO WA JULIUS NYERERE DAR ES SALAAM

      Comments Off on

KILELE CHA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KISAYANSI WA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO WA JULIUS NYERERE DAR ES SALAAM

Leo ikiwa ni kilele Cha mkutano wa kimataifa wa kisayansi wa magonjwa yasiyoambukiza katika ukumbi wa mikutano wa Julius Nyerere Dar es Salaam.

Katika mkutano huo madaktari kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road nao wamepata nafasi ya kuwasilisha mada zao.

Madaktari hao Ni Dkt. Harrieth Noah, Dkt. Felister Tupa na Dkt. Goodfrey Malangwa.

Pia wakati huo huo wa mikutano Banda la Taasisi ya Saratani Ocean Road limekuwa likitoa Elimu kuhusiana na Saratani.

Aidha ikumbukwe kuwa Taasisi ya Saratani Ocean Road hivi karibuni imepokea tuzo ya heshima ya kutambulika mchango wake katika kutoa elimu, kufanya uchunguzi na matibabu ya Saratani.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt.Julius Mwaiselage leo amepokea msaada wa millioni arobaini kutoka Bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT).

      Comments Off on

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt.Julius Mwaiselage leo amepokea msaada wa millioni arobaini kutoka Bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT).

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt.Julius Mwaiselage leo amepokea msaada wa millioni arobaini kutoka Bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT).

Bodi ya michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT) imetoa msaada huo katika kuadhimisha miaka ishirini ya Bodi hiyo ya michezo ya kubahatisha Tanzania.

Bodi hiyo imetoa bedside Mia moja zenye thamani ya Shilingi milioni ishirini na nne, Hundi yenye thamani ya Shilingi milioni kumi na tano pamoja na vifaa mbalimbali ikiwemo sabuni na maji.

Akitoa shukrani zake Dkt. Mwaiselage amesema msaada huo utakwenda kuimarisha maeneo ya ugonjwa, pamoja na kwa wagonjwa moja kwa moja.

Pia Dkt. Mwaiselage ameahidi msaada huo utakwenda pale ulipokusudiwa kwa Usimamizi madhubuti huku akitoa wito kwa wadau wengine kuleta misaada zaidi na milango ya Taasisi ipo wazi kupokea misaada mbalimbali.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bodi ya Michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT) Bw. James Mbalwe amesema katika kusaidia Jamii ni Jambo la lazima sio hiari, ndio mana wao wameamua kurudisha kile kidogo walichopata kwa jamii.

Bw. Mbalwe ameongeza kuwa kujitolea kwa kutoa misaada kwa pamoja italeta tija kubwa kwa Jamii inayotuzunguka.

Aidha Bodi hiyo ya Michezo ya kubahatisha Tanzania (GBT) imeambatana na wadau wa michezo hiyo ya kubahatisha nchini katika kutoa misaada hiyo.

AFISA MIRADI WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA NGUVU ZA ATOMIC BI.AZA KASHLAN AMESEMA

      Comments Off on AFISA MIRADI WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA NGUVU ZA ATOMIC BI.AZA KASHLAN AMESEMA

Afisa miradi wa shirika la kimataifa la nguvu za Atomic Bi.Aza Kashlan amesema kuwa pamoja na msaada wa mashine walizozitoa kipindi cha nyuma, ila bado wataendelea na kutoa misaada mbalimbali ikiwemo mashine kwa namna itakavyowezekana ili kurahisisha matibabu katika Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Bi. Kashlan amesema mapema mwakani kutakuwa na mradi mwingine mkubwa ambao wanategemea pindi ukikamilika watauleta hapa katika Taasisi hii.

Akizungumza katika majadiliano maalum yaliyofanyika katika ukumbi uliopo ofisini kwake, mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt Julius Mwaiselage amesema kuwa ujio wa kiongozi huyu umempa nafasi ya kuzungumza nae mambo mbalimbali ikiwamo, kuanzisha shahada ya uzamili kwenye fizikia tiba, ununuzi wa vifaa mbalimbali vya kitabibu mfano, mashine za tiba n.k pqmoja na mafunzo upande wa uchunguzi kwenye mambo ya CT Scan.

Bi. Kashlan ameahidi kuitekeleza miradi yote ambayo Dkt. Mwaiselage amemuomba pindi tu muda utakapofikia kwa kuanzia na mambo kadhaa mapema mwakani.

TAASISI YA SARATANI YA OCEAN ROAD IMEANZA KUTOA HUDUMA YA MIONZI TIBA YA NDANI KWA NJIA YA KISASA (3D INTRACAVITARY BRACHYTHERAPY)

      Comments Off on

TAASISI YA SARATANI YA OCEAN ROAD IMEANZA KUTOA HUDUMA YA MIONZI TIBA YA NDANI KWA NJIA YA KISASA (3D INTRACAVITARY BRACHYTHERAPY)

Taasisi ya Saratani ya Ocean Road imeanza kutoa huduma ya mionzi tiba ya ndani kwa njia ya kisasa (3D INTRACAVITARY BRACHYTHERAPY) kwa wagonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi.

Hayo yamesemwa wiki hili na Dkt Faraja Kiwanga ambaye ni daktari bingwa wa saratani kutoka kliniki ya Bima (HIC) alipokuwa akiwasilisha maada na kuitambulisha huduma hiyo ambayo imeanza kutolewa katika Taasisi kuanzia mnamo mwezi wa tano mwaka huu 2023.

Huduma hii ni ya kibingwa bobezi ambayo inatumia vifaa vya kisasa kuanzia kwenye kumuandaa mgonjwa, kumuwekea vifaa tiba kwa ajili ya mionzi, kutumia kipimo cha CT scan kuangalia kama vifaa tiba vimekaa mahali pake vizuri, pia kutumia picha za CT scan kufanya kontua kwenye sehemu ambapo ugonjwa upo na kufanya kontua kwenye ogani zinazokaribia eneo linalotakiwa kupata tiba ya kutosha na bila kuathiri ogani zilizokaribu, pia kutumia picha za CT scan kupanga tiba na kufanya mahesabu ya dozi ya mionzi tiba na kuhakikisha kuwa ugonjwa unatibiwa kwa ubora wa hali ya juu.

Akichangia maada hiyo Kaimu Mkuu wa Kliniki ya Bima, Dkt Emmanuel Lugina alisema, huduma hii ni muhimu sana hasa ikizingatia kuwa saratani ya mlango wa kizazi ni Saratani inayoongoza kwa idadi ya wagonjwa, hivyo wahudumu wa afya wanapowaona wagonjwa wajikite katika kuwafanyia uchunguzi (clinical examination) na pia kuweka kumbukumbu (documentation) ili kuweza kupanga aina ya mionzi tiba ambayo itamfaa mgonjwa na pia katika kuongeza tafiti katika eneo hili.

Naye Dkt Nuru Mlagalila alichangia kuwa huduma hii ya mionzi tiba ni muhimu kwa wagonjwa wetu wanaotufikia katika taasisi kwa kuwa wengi wa wagonjwa wanafika katika hatua ya pili na ya tatu, ambapo wakipata huduma hii watapata matokeo mazuri ya tiba.

Huduma hii inatolewa kwa ushirikiano wa daktari bingwa wa saratani (clinical Oncologist), Mfizikia Tiba (Medical Physicist), mtaalamu wa mionzi tiba (Radiation Therapist), na wauguzi (Brachytherapy Nurse).

Huduma hii inapatikana katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Block C kwenye chumba cha Mionzi ya Ndani kila siku kuanzia saa mbili na nusu asubuhi hadi saa kumi na moja jioni Jumatatu hadi Ijumaa.

Naibu waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel leo ametembelea Taasisi ya Saratani Ocean Road

      Comments Off on

Naibu waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel leo ametembelea Taasisi ya Saratani Ocean Road

Naibu waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel leo ametembelea Taasisi ya Saratani Ocean Road na kuzungumza na baadhi ya watumishi, huku akiupongeza uongozi wa Taasisi hiyo kwa kusimamia vizuri pesa zinazotolewa na serikali kwaajili ya miradi mbalimbali.

Dkt. Mollel amesisitiza kuwa ujenzi wa jengo mfano la Cyclotron ukiliangalia kwa nje unaweza Sema limegharimu kiasi kidogo sana cha pesa ila kwa ndani ndio utagundua thamani ya pesa iliyotumika kuwa inaendana na ubora na umadhubuti wa jengo lenyewe.

Dkt. Mollel ameomba uharaka wa umaliziaji wa jengo hilo ufanyike kwani watanzania wanahitaji huduma zake mapema iwezekanavyo huku serikali ikitaka uwekezaji wake uanze kuleta tija kwa wananchi.

Nae mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt Julius Mwaiselage, amemhakikishia Dkt. Mollel kumalizika mapema kwa ujenzi huo kwani kwa upande wa jengo limekamilika kwa Asilimia tisini na nane wakati mashine tayari zimekwishasimikwa kwa asilimia Mia moja huku ukisubiriwa utaratibu wa kuunganisha umeme pekee ili mashine hizo zianze kutumika kama inavyotakiwa.

Jengo hilo limekusanya mashine mbili kubwa ambazo ni PET-CT SCAN pamoja na CYCLOTRON (kiwanda cha kutengeneza mionzi) ambapo kwa sasa kwa Tanzania nzima kitakuwa ni kimoja tu, ambacho kitakuwa kikitengeneza mionzi ambayo itatumika kwa Taasisi huku mingine ikipelekwa kwenye hospitali nyingine kwaajili ya kusaidia wahanga wa huko. Kwa sasa Taasisi inanunua mionzi hiyo kutoka Afrika ya Kusini huku gharama zake zikiwa kubwa mno ukilinganisha na uwezo wa watanzania wenyewe, hivyo kukamilika kwa usimikaji huo kutakuwa msaada mkubwa sana kwa Tanzania na Afrika mashariki na kati kwa ujumla.

MAADHIMISHO YA SIKU YA SARATANI YA MATITI DUNIANI, 2023

      Comments Off on

MAADHIMISHO YA SIKU YA SARATANI YA MATITI DUNIANI, 2023

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewataka wananchi kufanya uchunguzi wa awali wa kupima Saratani ya Matiti ili kujua hali zao na kupata matibabu mapema kwa wenye changamoto hiyo

Waziri Ummy ameyasema hayo Octoba Mosi, 2023 wakati akimuwakilisha Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango kwenye Maadhimisho ya Mwezi wa Saratani ya Matiti yaliyofanyika katika viwanja vya Taasisi ya Saratani Ocean Road Jijini Dar es Salaam.

Waziri Ummy amesema Tanzania inakadiriwa kuwa na wagonjwa wapya wa Saratani takribani Elfu Arobaini na Mbili (42,000) kila Mwaka ndio wanafika katika vituo vya kutolea huduma za Afya.

Pia, Waziri Ummy amesema taarifa ya mwaka 2022/2023, inaonesha kuwa Taasisi ya Saratani Ocean Road ilihudumia wagonjwa wapya takriban 8,779 na asilimia 13 ya wagonjwa hao sawa na wagonjwa 1,141 walikuwa na Saratani ya Matiti.

Sambamba na hayo, Waziri Ummy amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Wizara ya Afya kufunga mashine za CT-Scan katika Hospitali zote za Rufaa za Mikoa na mashine za Ultrasound katika Hospitali zote za Halmashauri nchini.

Nae mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuimarisha matibabu kwa kutuletea vifaa tiba vya kutosha kwaajili ya uchunguzi wa Saratani mbalimbali ikiwamo PET-CT huku maahine ya Cyclotron ikiwepo kwaajili ya kuzalisha mionzi tiba itakayo tumika hapa kwenye Taasisi huku bakaa ikipangwa kupelekwa kwenye maeneo mengine kwaajili ya kusaidia watanzania wengine.

Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka ifikapo mwezi wa kumia mabapo watu duniani kote huungana kupingana na ushambulizi wa aina yoyote wa Saratani hii huku ikiwasaidia wananchi waliokwisha athirika na ugonjwa huo kupata matibabu

MAWASILIANO BAINA YA WATOA HUDUMA ZA AFYA NI MUHIMU KATIKA KUPATA VIPIMO SAHIHI VYA MGONJWA.

      Comments Off on

MAWASILIANO BAINA YA WATOA HUDUMA ZA AFYA NI MUHIMU KATIKA KUPATA VIPIMO SAHIHI VYA MGONJWA.

Mtaalamu wa Maabara wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Bw. Peter Mwevila amesema swala la mawasiliano baina ya watoa huduma za afya ni muhimu katika kupata vipimo sahihi vya mgonjwa.

Bw. Mwavila ameyasema hayo leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo katika majengo ya Taasisi ya Saratani Ocean Road alipokuwa akiwasilisha mada inayosema “Sample Collection” katika uwasilishaji wa “Continues Medical Education” (CME).

Aidha Bw. Mwevila ameongeza kuwa katika uchukuaji wa “sample” kutoka kwa mgonjwa ni lazima kuzingatia maelekezo ya kila kipimo kinachohitajika kwa kuwa kila kipimo kina utaratibu wake.

Pamoja na hayo Bw. Mwevila ameongeza kuwa iwapo sample imecheleweshwa kufikishwa kwenye maabara au “sample” imehifadhiwa katika kifaa kisicho sahihi, itabidi kuchukuliwa “sample” nyingine ili kupata vipimo hitajika.

Taasisi ya Saratani Ocean Road imekuwa ikitoa fursa kwa idara na vitengo vya ndani na nje ya Taasisi katika kuwasilisha mada mbalimbali kwa watumishi wake, ili waweze kujenga uelewa wa pamoja.

SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA MATIBABU YA NYUKLIA

      Comments Off on

SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA MATIBABU YA NYUKLIA

SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA MATIBABU YA NYUKLIA – DKT UBUGUYU.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania inayoongozwa na Mhe Dk.Samia Suluhu Hassan imeimarisha huduma za matibabu yuklia yakihusisha uchunguzi na tiba hasa katika Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Magonjwa yasiyo ya kuambukiza kutoka Wizara ya Afya, Dkt Omary Ubuguyu, ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika ufungzi wa mafunzo ya wataalamu wa tiba nyuklia kutoka nchi 15 barani Afrika yanayofanyika katika Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Akizungumza zaidi Dkt Ubuguyu amesema Serikali imeanza kuongeza uwezo katika kuimarisha teknolojia za kisasa katika uchunguzi na tiba magonjwa ya saratani nchini ikiwemo ununuzi wa mashine ya kisasa ya uchunguzi na tiba ya PET/CT scan katika Taasisi ya Saratani Ocean Road. Aidha mashine za awali zipo katika hospitali Bugando na Taasisi ya Saratani Ocean Road

Aidha, alieleza jitihada zaidi za Serikali ya Tanzania katika maandalizi ya kujenga kituo cha umahiri wa matibabu ya saratani nchini ambacho kitakuwa bora kuliko vyote Afrika.

Kwa upande wake, Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dk. Julius Mwaiselage amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka kipaumbele suala la kuboresha matibabu ya kansa katika Taasisi hiyo kwa kutoa fedha za kujenga miundombinu mbalimbali na kununua mashine mbalimbali za matibabu na vifaa tiba.

Dkt Mwaiselage, amesema kuwa mafunzo haya ya watalaamu yamefanyika kwa usimamizi wa Shirika la Nguvu za Atomu Duniani (IAEA) kwa kushirikiana na Taasisi ya Saratani Ocean Road, na kwamba IAEA inaitambua Taasisi kwa umahiri wake ndiyo maana mafunzo ya Afrika yanaletwa kufanyika katika Taasisi.

Nae daktari Bingwa wa Magonjwa ya Nyuklia wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dkt. Tausi Maftah, amesema kupitia Teknolojia hiyo wanafanya uchunguzi wa magonjwa mbalimbali ikiwemo Figo, Moyo, mifupa, na magonjwa ya njia ya chakula kwa kutumia Nyuklia isiyo na athari kwa binadamu kwa makundi mbalimbali wakiwemo watoto.

Alisema kuwa huduma hiyo ya matibabu nyuklia inq changamoto kubwa sana nchini kwetu hivyo mafunzo haya yatachochea uelewa na kuboresh huduma za matibabu