MKURUGENZI WA HUDUMA ZA TIBA KUTOKA WIZARA YA AFYA PROF. PASCHAL RUGAJO,MAPEMA LEO AMETEMBELEA KATIKA KITUO KIPYA KILICHOSIMIKWA MASHINE ZA CYCLOTRON PAMOJA NA PET-CT SCAN

      Comments Off on

MKURUGENZI WA HUDUMA ZA TIBA KUTOKA WIZARA YA AFYA PROF. PASCHAL RUGAJO,MAPEMA LEO AMETEMBELEA KATIKA KITUO KIPYA KILICHOSIMIKWA MASHINE ZA CYCLOTRON PAMOJA NA PET-CT SCAN

Mkurugenzi wa huduma za Tiba kutoka wizara ya Afya Prof. Paschal Rugajo, (Picha ya kwanza kushoto) mapema leo ametembelea katika kituo kipya kilichosimikwa mashine za Cyclotron pamoja na PET-CT SCAN na kujionea maendeleo ya ujenzi wa jengo na usimikaji namna unavyoendelea

Akizungumza katika matembezi hayo Prof. Rugajo amesema kuwa ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi huo huku akiuomba uongozi kusimamia kwa umakini ili kituo hicho kiweze kukamilika mapema na kuanza kutoa huduma kwa wananchi wa ndani na nje ya Tanzania.

Akizungumza zaidi, Prof. Rugajo amewataka viongozi kuhakikisha wanatuza rasilimali hizo ili zije kuwafaa watanzania na kuepukana na ugonjwa wa Saratani ambao katika kipindi cha hivi karibuni umeshika kasi katika kupoteza maisha ya Watanzania wengi sana

Kwa upande wake mkurugenzi wa kinga wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Crispin Kahesa, amemshukuru Prof. Rugajo kwa kuweza kupata muda na kutembelea katika jengo hilo na kumuahidi kuwa matumizi ya mashine hizo hayatochukua muda mrefu kuanza ili kuweza kuleta mabadiliko chanya katika Tasnia ya uchunguzi na matibabu ya Saratani nchini

Aidha Dkt. Kahesa amemuhakikishia Prof. Rugajo kuwa mashine hizo zitabaki kuwa salama na zitatoa huduma kwa mujibu wa zinavyotakiwa kutoa kwani Taasisi imejipanga kuhakikisha kuwa inaendana na Sera ya nchi katika kutokomeza magonjwa mbalimbali ikiwemo ugonjwa huu wa Saratani mbalimbali

Wakati huohuo Dkt kahesa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuchagua kuwekeza kwenye afya kwa kiasi kikubwa, hasa kwa kuziwezesha Taasisi za kiserikali kuweza kutoa huduma za Afya hapa nyumbani kwa urahisi zaidi ili kupunguza rufaa zinazogharimu pesa nyingi za watanzania ambao wengi wao huishia kupoteza maisha kutokana na kushindwa kumudu gharama za matibabu nje ya nchi.

Mashine ya PET-CT Scan ni mashine yenye uwezo wa kugundua Saratani katika hatua za awali kabisa na hivyo kurahisisha matibabu na kuepuka madhara makubwa kwa watanzania hivyo kuwaepusha kufika hospitali wakiwa katika hatua za Tatu au nne ambazo ndio hatari sana kwani matibabu yake Yana changamoto za gharama ukilinganisha na yale ya hatua za mwanzo kabisa

USIMIKAJI WA MASHINE YA PET/CT SCAN UMEFIKIA HATUA NZURI AMBAPO VIFAA VYOTE VYA MSINGI

      Comments Off on

USIMIKAJI WA MASHINE YA PET/CT SCAN UMEFIKIA HATUA NZURI AMBAPO VIFAA VYOTE VYA MSINGI

Usimikaji wa mashine ya PET/CT Scan umefikia hatua nzuri ambapo vifaa vyote vya msingi vimekamilika na kubakia kuunganisha mfumo wa umeme na vifaa vichache ili iweze kufanya kazi kama inavyotarajiwa.

Mashine hiyo ya PET/CT Scan ni utekelezaji wa maono ya Rais Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania katika kuboresha huduma za saratani nchini.

Mradi huu ulihusisha ujenzi wa jengo maalum la kusimika mashine za PET/CT Scan na Cyclotron, ambapo mpaka sasa mradi huo umegharimu kiasi cha Shilingi bilioni 18.2.

Mashine hiyo ambayo inatarajia kuanza kufanya kazi hivi karibuni, inauwezo mkubwa wa kugundua Saratani hata ikiwa katika hatua za awali kabisa.

Mashine hii pindi itakapokamilika, itasaidia kupunguza gharama kwa watanzania kwenda nje ya nchi huku ikitarajiwa kupokea wageni wengi zaidi kutoka nchi mbalimbali barani Afrika, kwani ni miongoni mwa mashine chache sana zenye uwezo mkubwa katika Bara hili.

MAFUNZO KWA WATUMISHI WAPYA WA UMMA KATIKA AASISI YA SARATANI OCEAN ROAD

      Comments Off on

MAFUNZO KWA WATUMISHI WAPYA WA UMMA KATIKA AASISI YA SARATANI OCEAN ROAD

Mkurugenzi wa utawala na Rasilimali watu wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Bi. Beatrice Erasto kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt.Julius Mwaiselage amewapa vyeti watumishi wapya Leo baada ya kuhitimu Mafunzo.

Mafunzo hayo ya utumishi wa umma yamefanyika kwa muda wa siku tano katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo katika majengo ya Taasisi ya Saratani Ocean Road.

ORCI, YAPELEKA MADAKTARI INDIA KUJIFUNZA ZAIDI.

      Comments Off on

ORCI, YAPELEKA MADAKTARI INDIA KUJIFUNZA ZAIDI.

Taasisi ya Saratani Ocean Road imepeleka madaktari wake bingwa India huku lengo la safari hii ni kuwajengea uwezo madaktari na kuifanya Tanzania kuwa kituo cha Tiba utalii kwa nchi za Kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Taasisi imewakilishwa na Dkt Caroline Swai, Daktari bingwa wa magonjwa ya Saratani, Dkt. Revelian Iramu Daktari bingwa wa radiolojia na Dkt. Bright Sangiwa Daktari bingwa wa mionzi Tiba kutika Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Madaktari hawa wamepata fursa ya kutembelea Hospitali za Apollo, YASHODA, HCG, Sakra, BLK-Max, Fortis na Hospitali ya chuo kikuu cha Sharda na kujifunza mambo mengi ambayo watapata fursa ya kuja kuyatumia katika Taasisi hii.

Huu ni mpango madhubuti ulioasisiwa na serikali ili kuweza kuwapa ujuzi baadhi ya madaktari wa Hospitali na Taasisi zote za serikali ili waweze kuisaidia Tanzania katika sekta ya Afya nchini pamoja na walio nje ya Tanzania ambao huja kutibiwa nchini.

MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD DKT. JULIUS MWAISELAGE AMESEMA MAAZIMIO KARIBU YOTE YALIYOWEKWA KATIKA KIKAO KILICHOPITA CHA BARAZA YAMEKAMILIKA

      Comments Off on

MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD DKT. JULIUS MWAISELAGE AMESEMA MAAZIMIO KARIBU YOTE YALIYOWEKWA KATIKA KIKAO KILICHOPITA CHA BARAZA YAMEKAMILIKA

Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt. Julius Mwaiselage amesema maazimio karibu yote yaliyowekwa katika kikao kilichopita Cha Baraza yamekamilika na kubaki maazimio machache ambayo yapo katika utekelezaji.

Hayo yamesemwa Katika kikao cha sita cha Baraza la Tano la wafanyakazi wa Taasisi ya Saratani Leo ndio ikiwa inakamilisha muda wake wa miaka mitatu.

Kikao hicho kimejadili Mambo mbalimbali ya Taasisi pamoja na mustakabali wa wafanyakazi wa Taasisi katika kuendeleza gurudumu la Maendeleo ya Taifa la Tanzania.

Dkt. Mwaiselage amesema kuwa Taasisi inaendelea kutoa huduma zote zinazotolewa katika Taasisi hiyo ikiwemo huduma za Kinga, huduma za uchunguzi, huduma za Tiba Mionzi na huduma nyinginezo.

Aidha Dkt. Mwaiselage amethibitisha kuwa Taasisi hiyo ipo salama isipokuwa kuna changamoto ndogo za kiubinadamu ambazo ameahidi kuzishughulikia na kuzimaliza kabisa.

Kutokana na Baraza hilo kufanya majukumu yake kwa muda wote wa miaka mitatu bila migogoro na kukubaliana Mambo yote ya Maendeleo katika Taasisi ya Saratani, kila mjumbe wa Baraza hilo ametunukiwa tuzo, ikiwa ni ishara ya kutambua mchango mkubwa wa kila mjumbe kwenye kujali maslahi ya wafanyakazi katika baraza hilo

Pamoja na hayo Dkt. Mwaiselage amewataka wajumbe watakaochaguliwa tena kwenye Baraza la Sita kumpa ushirikiano zaidi katibu atakayekuwepo katika Baraza lijalo.

WAJUMBE WA KAMATI YA UTEKELEZAJI WILAYA,JUMUIYA YA WAZAZI WA CCM IKIONGOZWA NA MWENYEKITI WA TAASISI YA MWALIMU NYERERE FOUNDATION WAMEFANYA ZIARA MAALUM KATIKA TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD

      Comments Off on

WAJUMBE WA KAMATI YA UTEKELEZAJI WILAYA,JUMUIYA YA WAZAZI WA CCM IKIONGOZWA NA MWENYEKITI WA TAASISI YA MWALIMU NYERERE FOUNDATION WAMEFANYA ZIARA MAALUM KATIKA TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD

Wajumbe wa kamati ya utekelezaji wilaya, jumuiya ya wazazi wa chama Cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Ilala ikiongozwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation Mhe. Joseph. W. Butiku Leo mapema wamefanya ziara maalum katika Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Katika ziara hiyo Mh. Butiku ameshiriki na viongozi wengine wa Jumuiya ya wazazi wa CCM na Taasisi ya Saratani katika kupanda miti ya kivuli katika maeneo ya Taasisi ya Saratani.

Jumuiya ya wazazi wilaya ya Ilala imefanya ziara hiyo katika kuadhimisha wiki ya wazazi kitaifa.

Aidha Mhe. Butiku ameupongeza uongozi wa Taasisi ya Saratani Ocean Road kwa kazi nzuri zinazofanyika katika kuwahudumia wagonjwa.
Mhe. Butiku ameendelea kusema kuwa kazi inayofanywa na Serikali katika kujenga majengo, huduma, ununuzi wa vifaa pamoja na madawa, hayo yote ni katika kudumisha amani, kudumisha umoja na kuleta maendeleo ya watu wote.

Pamoja na hayo Mhe. Butiku amesema PET/CT Scan ndio yenyewe katika uchunguzi na sasa imekwisha fika katika Taasisi ya Saratani, tuipongeze serikali yetu kwa kuleta mashine hiyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani Dkt. Julius Mwaiselage amesema Taasisi ya Saratani kupitia serikali ya Jamuhuri ya Tanzania inatekeleza miradi ya maendeleo kutokana na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kutokana na uboreshaji wa miundombinu uliofanywa na Serikali katika eneo la matibabu na uchunguzi wa kibingwa na ubingwa bobezi, Rufaa za matibabu nje ya nchi zimepungua. Na itakapokamilika kwa usimikaji wa PET/CT Scan pia itasaidia wale wagonjwa wa Rufaa kwa ajili ya mashine hiyo kupata huduma hizo hapa hapa nchini amesema Dkt. Mwaiselage.

Aidha Dkt. Mwaiselage amesema kuwa Taasisi kwa hivi sasa ina mashine nne za Tiba Mionzi. Na kwa hivi sasa wagonjwa ni wengi wenye mahitaji ya tiba mionzi.

Hivyo Taasisi inahitaji kuongeza mashine nyingine nne ili kukidhi mahitaji ya wagonjwa kwa ufanisi wa hali ya juu kabisa.

Pamoja na hayo Dkt. Mwaiselage ameishukuru jumuiya ya wazazi kwa kufanya ziara katika Taasisi ya Saratani na kutoa ahadi ya kusimamia miti kwa kuitunza miti hiyo iliyopandwa.

ORCI YATOA SOMO KUHUSU SARATANI KWA WAHUDUMU WA AFYA LINDI.

      Comments Off on

ORCI YATOA SOMO KUHUSU SARATANI KWA WAHUDUMU WA AFYA LINDI.

ORCI YATOA SOMO KUHUSU SARATANI KWA WAHUDUMU WA AFYA LINDI.

Na Mwandishi wetu

Taasisi ya Saratani Ocean Road, leo imetoa somo kuhusu Saratani kwa baadhi ya wahudumu wa Afya kutoka katika hospitali ya Rufaa ya Sokoine.

Akitoa somo hilo kwa kushirikiana na baadhi ya madaktari, Dkt. Maguha Stephano amesema kwa sasa ugonjwa huu umeendelea kuwa hatari kitu kinachofanya Taasisi kuendelea kuwekeza kwa kununua mitambo ya kisasa ili kuweza kusaidia wananchi kulingana na matatizo yao.

Aidha Dkt. Maguha amewaeleza whudumu hao wa Afya kuwa pamoja na uhatari wa Saratani lakini unatibika hivyo amewasisitiza kuwaeleza wagonjwa kuwa waweze kufika kufanya uchunguzi mapema ili ikiwa atagundulika mapema basi aweze kufanyiwa rufaa kufika Taasisi ya Saratani Ocean Road kwaajili ya uchunguzi zaidi na matibabu.

Pia Dkt Maguha amesema kwa watanzania hii ni fursa kubwa kuitumia kwani kama nchi nyingine za Afrika wanaitumia kwa kuweza kuja na kutibiwa kutokana na uwekezaji wa Serikali ya awamu ya Sita inayoongzwa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwanini sio wenye nchi yao, hivyo amesisitiza kuitumia fursa hiyo ili kuepukana na hatari inayoweza ikajitokeza.

Taasisi ya Saratani Ocean Road inatekeleza Agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuwatembelea wananchi walioko pembezoni na kuwapa huduma hizi bila malipo yoyote, hivyo katika uchunguzi wa hatua za awali kwa mikoa yote ambayo Taasisi itapita itatoa huduma hizi bila malipo yoyote ambapo kwa mwezi huu Taasisi ipo Lindi kwaajili ya kufanya uchunguzi wa Saratani za Matiti, Mlango wa kizazi kwa wakina mama pamoja na Tezi Dume kwa wakina baba na baadae Tarehe 07/05/2023 timu hiyo itaelekea Mtwara kwa kutoa huduma hizo hizo mpaka tarehe 12/05/2023, huku mpango huu ukiwa umewekwa vizuri ili kila mwezi kuwe na mkoa mmoja au miwili ambayo itatembelewa na kupewa huduma hizo.

Dkt Mwaiselage akabidhi Makombe kwa bodi ya udhamini.

      Comments Off on

Dkt Mwaiselage akabidhi Makombe kwa bodi ya udhamini.

Dkt Mwaiselage akabidhi Makombe kwa bodi ya udhamini.

Na Mwandishi wetu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Dkt Julius Mwaiselage amekabidhi makombe matatu yaliyopatikana katika mashindano ya MEI MOSI kwa Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini katika Taasisi hiyo Prof. Ephata Kaaya.

Akizungumza katika makabidhiano hayo Dkt. Mwaiselage amesema kuwa katika Taasisi hii wanamichezo wamekuwa wakijitoa kwa hali na mali ili kuweza kuleta heshima katika Taasisi hii.

Akiendelea Dkt. Mwaiselage amesema kuwa kwa miaka takribani mitatu mfululizo wamekuwa wakirudisha makombe zaidi ya matatu huku wakiitangazq Taasisi kwa ushindi wa wa jumla ambapo kwa mwaka huu wamejinyakuliq ushindi wa tatu kwenye ushindi wa jumla kwa kuvuna point 7.

Nae Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini wa Taasisi hiyo prof. Ephata kaaya ameupongeza uongozi wa Dkt. Julius Mwaiselage kwa kuendelea kusimamia vyema swala la michezo katika Taasisi pamoja na kazi nyingi na ngumu wanazoendelea kuzifanya.

Akipokea makombe hayo Prof. Kaaya amesema bodi yake ipo tayari kushirikiana na wanamichezo wote na inaendelea kuwatia nguvu zaidi ili wakati mwingine waweze kuleta makombe zaidi ya hayo matatu.

Prof. Kaaya amesisitiza kuwa, wafanyakazi wanapomaliza kazi zao wakumbuke kufanya mazoezi kwaajili ya Afya zao lakini pia kusaidia kusukuma mbele gurudumu la kimichezo kwa Taasisi ili kuweza kujipatia sifa na kuitangaza taasisi kwa shughuli za kimichezo na kimatibabu.

TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD LEO KATIKA KILELE CHA MAAZIMISHO YA SIKU YA MWANAMKE DUNIANI IMEPOKEA MISAADA MBALIMBALI KUTOKA KWA WANAWAKE WA TAASISI NA IDARA MBALIMBALI

      Comments Off on

TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD LEO KATIKA KILELE CHA MAAZIMISHO YA SIKU YA MWANAMKE DUNIANI IMEPOKEA MISAADA MBALIMBALI KUTOKA KWA WANAWAKE WA TAASISI NA IDARA MBALIMBALI

Taasisi ya Saratani Ocean Road leo katika kilele Cha maazimisho ya siku ya Mwanamke Duniani imepokea misaada mbalimbali kutoka kwa wanawake wa Taasisi na idara tofauti tofauti hapa nchini Tanzania kwa ajili ya wagonjwa.

Msimamizi wa Kitengo cha Ustawi wa Jamii wa Taasisi ya Saratani Ocean Road Bi. Devotha Kovaga amesema wanawake wameleta misaada tofauti tofauti ikiwemo viti vya kuwabebea wagonjwa, Sabuni, Dawa za meno, pesa taslimu kwa baadhi ya wagonjwa na vitu vingine vidogo vidogo vya kuwasaidia wagonjwa katika mahitaji yao. Pia wakina mama hao wamewanunulia wagonjwa dawa kwa wale ambao siku ya Leo wamekuwa na changamoto ya kugharamia dawa.

Aidha Bi. Kovaga amesema makundi ya wanawake hao ni wanawake kutoka Benki ya Maendeleo ya kilimo (TADB), wanawake kutoka kampuni ya Said Salim Bakhresa Co. Ltd, wanawake kutoka Maabara ya Taifa, wanawake kutoka TCRA, wanawake kutoka Airport pamoja na wanawake kutoka Mamlaka ya mapato idara ya walipa Kodi wakubwa.

Pamoja na hayo Bi. Kovaga ametoa shukrani kwa wadau wote waliotoa misaada hiyo na kutoa wito kuwa wagojwa wanaitaji misaada ya mara kwa mara, hivyo wanakaribishwa muda wowote kuja na kutoa misaada.
Na amesisitiza kuwa ugonjwa wa Saratani inatibika, muhimu ni kufanya uchunguzi wa mara kwa mara na kupata tiba sahihi.

MKURUGENZI MTENDAJI WA TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD, DKT. JULIUS MWAISELAGE, AMEWATAKA WANAWAKE KATIKA TAASISI HIYO KUFANYA KAZI KWA BIDII…

      Comments Off on

MKURUGENZI MTENDAJI WA TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD, DKT. JULIUS MWAISELAGE, AMEWATAKA WANAWAKE KATIKA TAASISI HIYO KUFANYA KAZI KWA BIDII…

Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Dkt. Julius Mwaiselage, amewataka wanawake katika Taasisi hiyo kufanya kazi kwa bidii na kufuata misingi ili kuweza kupata mafanikio zaidi kwenye maisha yao.

Akizungumza wakati akitoa salamu zake za siku ya wanawake Duniani Dkt. Mwaiselage amesema kuwa msingi ulio imara na ambao ndio nguzo thabiti kwenye kila maendeleo ni kufanya kazi kwa juhudi na kufuata misingi kwenye shughuli anayofanya.

Aidha Dkt mwaiselage amewaasa wanawake wa hapa kushirikiana katika kuwasaidia wanawake wengine hasa kwenye tatizo hili la Saratani ya Matiti na mlango wa kizazi ili kuweza kuokoa kina mama wengi ndani na nje ya nchi

Dkt. Mwaiselage amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambae ndie amewezesha kwa kiwango kikubwa upatikanaji wa mashine nyingi za kusaidia uchunguzi ikiwamo mammogram, MRI na mashine nyingine nyingi ambazo zitasaidia kurahisisha uchunguzi wa Saratani katika Taasisi hiyo.

Kila inapofika Tarehe 08/03/ ya kila mwaka, huwa ni siku ya wanawake duniani ambapo wanawake kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road husherehekea kwa namna yake ikiwamo kutoa Jumbe mbalimbali zinazosaidia kinamama kuutambua ugonjwa wa Saratani hususan Saratani ya Mlango wa kizazi na Matiti.